KINDIKI ASEMA UCHAGUZI 2027 UTAAMULIWA NA MAENDELEO
Naibu Rais Kithure Kindiki ametetea rekodi ya maendeleo ya serikali akisema uchaguzi mkuu ujao utaamuliwa na utendakazi pamoja na utoaji huduma badala ya siasa za maneno.
Akizungumza katika eneo Bunge la Msambweni, Kindiki amesema serikali ya Kenya Kwanza inalenga kubadilisha maisha ya wananchi kupitia miundombinu, umeme, masoko na uchumi wa baharini.
Amesisitiza kuwa Rais William Ruto atatafuta muhula wa pili kwa msingi wa maendeleo yaliyotekelezwa katika sekta za barabara, umeme, bandari na masoko.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































