#Local News

NJERI MAINA ATAKA HATUA ZA DHARURA DHIDI YA MAUAJI YA WANAWAKE

Mwakilishi wa Wanawake wa Kaunti ya Kirinyaga Njeri Maina ametaka kuwepo kwa hatua za haraka na za pamoja kitaifa kukabiliana na ongezeko la mauaji ya wanawake na watoto wanaopotea nchini.

Katika taarifa yake, Maina amesema visa vinavyoongezeka vya wanawake kuuawa na watoto kutoweka vinaonyesha kuwa taifa linakabiliwa na janga kubwa linalohitaji ushirikiano wa taasisi zote za serikali pamoja na jamii.

Aidha amesema juhudi zilizopo kwa sasa bado hazijaratibiwa ipasavyo na mara nyingi huwa za kuitikia matukio badala ya kuzuia matatizo hayo mapema.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *