WANNE WAFARIKI KWENYE JENGO SHAURI MOYO
Shughuli za uokoaji zinaendelea mtaani Shauri Moyo jijini Nairobi ambako jumba moja limeporomoka na kuwaua watu 4 huku wengine 4 wakiokolewa.
Kwa mujibu wa wizara ya usalama wa kitaifa, jumba hilo ni miongoni mwa mijengo inayoendelea kubomolewa na tume inayosimamia uimarishaji wa Nairobi River katika eneo la Blue Estate, karibu na mto huo.
Watu zaidi wanahofiwa kukwama kwenye jengo hilo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































