KINDIKI AWAHIMIZA WAKENYA KUJISAJILI KAMA WAPIGA KURA
Naibu Rais, Kithure Kindiki, amewataka Wakenya ambao bado hawajasajiliwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika orodha ya wapigakura kabla ya muda uliowekwa kukamilika.
Kindiki amesema kuwa wale watakaoshindwa kujiandikisha hawatakuwa na uwezo wa kuchagua viongozi wanaowataka katika uchaguzi ujao.
Akizungumza katika kaunti ya Tharaka Nithi, wakati wa sherehe za Pasaka, Naibu Rais amewahimiza wananchi kuchukua hatua mapema ili kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kidemokrasia.
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































