#Sports

KSSA: ST ANTONY’S YAIBUKA NA USHINDI KWENYE MAGONGO

Shule ya St Antony’s ya Kitale imeanza vyema mashindano ya kitaifa ya michezo ya shule za upili muhula wa kwanza baada ya kuibuka na ushindi dhidi ya wenyeji Kisumu Day.

Katika mchezo huo uliokuwa mkali, nyota wa timu hiyo Kevin Onyango alifunga bao pekee lililoipa ushindi wa bao moja kwa bila dhidi ya wapinzani wao.

Kocha wa timu hiyo Kevin Lugalia amesema wanapania kurejesha ubingwa waliotwaa mwaka 2022 huku wakijiamini kuendelea vyema katika mashindano hayo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *