WAUGUZI KNH KUANZA MGOMO
Huenda huduma za matibabu katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta zikatatizika kuanzia leo kutokana na mgomo wa wauguzi, wanaodai kwamba mishahara yao imecheleweshwa.
Katibu mkuu wa muungano wa kitaifa wa wauguzi, Seth Panyako, amelalamikia madai hayo akiongeza kuwa malipo ya uzeeni hayajalipwa na kwamba wauguzi wanahudumu kwa kandarasi bila kupewa ajira ya kudumu zaidi ya muda unaostahili.
Tayari tangazo la mgomo kwenye hospitali hiyo kubwa nchini limeibua hofu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































