WAUGUZI, WAKUNGA KNH WASITISHA MGOMO
Utoaji wa huduma za matibabu katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta umerejelea hali ya kawaida baada ya wauguzi kusitisha mgomo wao kufuatia mazungumzo kati ya usimamizi wa hospitali hiyo na muungano wa wauguzi na wakunga.
Akitoa tangazo hilo, Waziri wa afya Aden Duale amesema mkataba huo uliafikiwa baada ya pande husika kujitolea kwa mazungumzo ya kutamatisha mgomo huo.
Mgomo huo ulianza Jumatatu wiki hii, wauguzi wakilalamikia masuala kadhaa ikiwemo mzigo wa kazi kutokana na uhaba wa wauguzi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































