BEI YA MAFUTA: RUTO ATAKIWA KUPANDISHA MISHAHARA
Rais William Ruto ametakiwa kupandisha kiwango cha chini cha mishahara ya wafanyakazi wa ngazi ya chini kutokana na kupanda kwa gharama ya maisha.
Katibu mkuu wa muungano wa vyama vya wafanyakazi, COTU, Francis Atwoli, amesema kuwa ongezeko la bei ya mafuta litapandisha gharama hiyo moja kwa moja.
Ametaka hatua hiyo kutangazwa rasmi kabla ya maadhimisho ya Leba dei mwezi ujao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































