#Football #Sports

EMILY ADHIAMBO AIAMINI JUNIOR STARLETS DHIDI YA UGANDA

Mshambuliaji wa Junior Starlets Emily Adhiambo amesema ana imani Kenya itaifunga Uganda katika mechi ya marudiano ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la Wanawake chini ya miaka 17 itakayochezwa hapo kesho katika uwanja wa Nyayo.

Kenya ilipata sare muhimu ya mabao 1-1 dhidi ya Uganda  katika mkondo wa kwanza uliochezwa Kampala, ambapo Adhiambo alifunga bao la kusawazisha baada ya Uganda kuongoza mapema kupitia Shadia Nabirye.

Adhiambo amesema matokeo hayo yameipa timu morali na kujiamini kuelekea mchezo wa marudiano, huku akisisitiza kuwa wachezaji wako tayari kutumia faida ya kucheza nyumbani kuhakikisha wanafuzu hatua inayofuata ya mashindano hayo makubwa duniani.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *