#uncategorized

TUZO YA BALLON D’OR KUFANYIKA LONDON

Sherehe za utoaji wa tuzo ya Ballon d’Or mwaka 2026 zitafanyika kwa mara ya kwanza jijini London Oktoba 26 kuadhimisha miaka 70 tangu tuzo hiyo ilipotolewa kwa mara ya kwanza mwaka 1956.

Waandalizi wamesema hafla hiyo itaadhimisha kumbukumbu ya mwanasoka wa Uingereza Stanley Matthews aliyekuwa mshindi wa kwanza wa tuzo hiyo.

Katika miaka ya hivi karibuni, tuzo hiyo imekuwa ikitawaliwa na Lionel Messi na Cristiano Ronaldo huku mshambuliaji wa Paris Saint-Germain Ousmane Dembele akitwaa tuzo hiyo mwaka uliopita.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *