TUWASHAURI WATOTO

Baadhi ya viongozi wa kidini wanaitaka serikali kupitia wizara ya elimu kuwapa ushauri nasaha wanafunzi ambao jamaa zao walifariki au kujeruhiwa katika janga la mafuriko.
Mwenyekiti wa kanisa la Kenya Evangelical Alliance tawi la Nandi Teddy Kisivuli amesema ni vyema kwa wanafunzi na walimu kupewa ushauri nasaha ili kuepuka msongo wa mawazo hasa shule zinapofunguliwa Jumatatu wiki ijayo.
English 




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































