AFUENI KWA WANABODI YA UMMA KAKAMEGA
Wanachama 4 wa bodi ya huduma za umma katika kaunti ya Kakamega waliokuwa wamesimamishwa kazi wamepata afueni baada ya mahakama kuagiza kwamba warejee kazini na kufidiwa shilingi milioni moja kila mmoja kutokana na mahangaiko waliopitia.
Hata hivyo, gavana wa kakamega Fernandez Barasa kupitia kwa wakili wake Patrick Lutta, ametuma ombi la kuwazuia kurejea afisini akijiandaa kukata rufaa kupinga uamuzi huo.
Wanne hao ni Catherine Omweno, Stanley Were, Rapha Wangatia na Joel Omukoko.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































