#Local News

AFUENI KWA WANABODI YA UMMA KAKAMEGA

Wanachama 4 wa bodi ya huduma za umma katika kaunti ya Kakamega waliokuwa wamesimamishwa kazi wamepata afueni baada ya mahakama kuagiza kwamba warejee kazini na kufidiwa shilingi milioni moja kila mmoja kutokana na mahangaiko waliopitia.

Hata hivyo, gavana wa kakamega Fernandez Barasa kupitia kwa wakili wake Patrick Lutta, ametuma ombi la kuwazuia kurejea afisini akijiandaa kukata rufaa kupinga uamuzi huo.

Wanne hao ni Catherine Omweno, Stanley Were, Rapha Wangatia na Joel Omukoko.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *