IPOA YATISHIA KUELEKEA MAHAKAMANI
Mamlaka ya kutathmini utendakazi wa Polisi (IPOA) inataka kaimu Inspekta Jenerali wa Polisi Douglas Kanja na Kamanda wa Polisi wa Nairobi Adamson Bungei wakamatwe kutokana na mienendo yenye kutiliwa shaka ya polisi iliyoshuhudiwa wakati wa maandamano ya nchi nzima.
Kamishna wa IPOA John Waiganjo amesema kwamba mamlaka hiyo inasikitishwa na ukosefu wa taaluma unaoonyeshwa na maafisa wa polisi wanapowahusisha waandamanaji katika muda wa wiki nne zilizopita na sasa wanazidisha suala hilo katika Mahakama.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































