WALIMU WAANDAMANA NAIROBI, WAAPA MGOMO UNGALIPO
Walimu wa shule za sekondari wamelemaza masomo kwa siku ya 5 mfululizo kote nchini wakiitaka tume ya kuwaajiri walimu TSC itekeleze mkataba wa maelewano wa kati ya mwaka 2021-25 ikiwemo kuwapa makataba wa kudumu walimu wa JSS.
Jijini Nairobi, walimu hao wameandamana hadi katika afisi za TSC wakisisitiza kwamba mgomo utaendelea hadi mkataba wao utekelezwe.
Aidha, muungano wa walimu hao KUPPET umeikosoa TSC kwa kuwataka waandike barua ya kuitisha mazungumzo na kisha kuichapisha barua hiyo mitandaoni.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































