MASAIBU YA MOI YAKOSA KIKOMO
Huenda shughuli za masomo zikakosa kurejelewa katika chuo kikuu cha Moi baada ya wahadhiri wa chuo hicho kuapa kuendelea na mgomo wao ambao umedumu kwa miezi 3, licha ya chuo hicho kuwataka wanafunzi warejee wiki ijayo.
Kwa mujibu wa wahadhiri hao, watarejea kazini tu iwapo wizara ya elimu itakubali ombi lao la kutaka usimamizi mpya chuoni humo, mbali na kulipwa kwa mishahara yao kikamilifu.
Aidha, wamesema kuwa masaibu ya chuo hicho ikiwemo madeni ya takribani shilingi bilioni 9 yanmesababishwa na usimamizi mbaya na utumizi mbaya wa fedha.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































