WAKENYA HALISI KUPOKEA VITAMBULISHO

Rais William Ruto amefafanua kwamba mageuzi ya serikali kuhusu utoaji wa vitambulisho vya kitaifa hayakufuta uthibitishaji wa uraia, akisisitiza kwamba ni raia halali wa Kenya pekee watakaopokea hati hizo. Akizungumza wakati wa sherehe za siku ya madaraka katika kaunti ya Wajir hii leo, Ruto amesema mageuzi yaliyoanzishwa na utawala wake yanalenga kukomesha ubaguzi dhidi ya jamii […]

SHEREHE ZA MADARAKA

Rais william ruto amewasili katika uwanja wa Wajir kwa ajili ya sherehe za siku ya madaraka ya 2026, ikiwa ni mara ya kwanza kwa hafla ya kitaifa kufanyika katika eneo la kaskazini mashariki mwa Kenya. Maadhimisho ya siku ya madaraka ya mwaka huu yatafanyika chini ya kaulimbiu, “elimu, ujuzi na mustakabali,”  huku serikali ikisema tukio hilo linalenga […]

LINDA MWANANCHI KUELEKEA THIKA

Mrengo wa Linda Mwananchi unatarajiwa kufanya mkutano wa mashauriano mjini Thika huku ukiongeza juhudi za kupanua ushawishi wake kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027. Akizungumza katika mkutano wa kisiasa Kaunti ya Machakos Mbunge wa Suba Kusini Caroli Omondi amesema muungano huo una uwezo wa kujikusanyia hadi kura milioni 16 katika uchaguzi ujao. Mkutano wa Thika utakuwa wa […]

SERIKALI KUPANGA MAZISHI YA WANAFUNZI 16

Serikali imeunda kamati maalum ya kuratibu mazishi ya wanafunzi 16 waliofariki katika mkasa wa moto uliotokea katika shule ya Utumishi Girls Academy wiki iliyopita. Kwa mujibu wa afisa mmoja wa kamati hiyo, mwelekeo wa maandalizi hayo utatangazwa Jumanne, huku serikali ikiahidi kugharamia mazishi ya waliofariki pamoja na matibabu ya wanafunzi wanaoendelea kupokea huduma hospitalini. Hatua […]

UPINZANI WATAKA KATIBA IHESHIMIWE

Viongozi wa muungano wa upinzani wameitaka marekani kuheshimu Katiba ya Kenya pamoja na kutii amri za mahakama zilizositisha mpango wa kuanzisha kituo cha karantini ya Ebola nchini. Viongozi hao wamesema hatua yoyote inayohusu kuanzishwa kwa kituo hicho inapaswa kufuata sheria za nchi na kuhusisha wananchi kupitia mchakato wa ushirikishwaji wa umma. Aidha, wamependekeza kufanyika kwa kikao cha […]