YUSUF HASSAN MBUNGE WA KAMUKUNJI AMESAMBAZA CHAKULA CHA MSAADA KWA WAADHIRIWA WA MAFURIKO

Mbunge wa Kamukunji Yusuf Hassan amesambaza chakula kwa zaidi ya watu 10,000 wote wakiwa waadhiriwa wa janga la mafuriko katika eneo bunge hilo. Akizungumza katika kituo cha usambazaji maji eneo bunge Yusuf amesikitika kwamba mafuriko makubwa yaliyoshuhudiwa katika siku chache zilizopita yameacha athari mbaya kwa familia na watoto wanaoenda shule. Mafuriko hayo yameifanya sehemu ya […]

RUTO ANYIMWA NAFASI KULIHUTUBIA BUNGE LA MAREKANI

Rais William Ruto hatahutubia kikao cha pamoja cha Congress katika ziara yake ijayo ya Kiserikali nchini Marekani. Hii ni baada ya Spika Mike Johnson kukataa ombi la baadhi ya wabunge wa Democrat waliokuwa wamemwalika Rais Ruto kuhutubia bunge la kitaifa la marekani. Katika taarifa naibu mkuu wa wafanyikazi wa Spika Johnson Raj Shah amesema uamuzi […]

ABIRIA WAKWAMA NDANI YA GARILA ABIRIA KWENYE AJALI JOGOO ROAD

Baadhi ya abiria wamekwama ndani ya basi lilioanguka katika eneo la makutano buruburu kwenye barabara ya Jogoo Rd. Basi hilo la kampuni ya Forward lililokuwa linaelekea katikati ya jiji la Nairobi kutoka mtaa wa kayole wakati lilipoanguka na kusababisha msongomano wa magari. Maafisa wa polisi wa trafiki Pamoja na maafisa wa huduma za dharura kwa […]

ELIZABETH CHESANG TATU TENA

Mwenyekiti wa baraza la watu wenye ulemavu NCPD Elizaeth Chesang ameongezewa muda wa kuhudumu katika wadhfa huo kwa miaka mitatu Zaidi, Chesang ambaye alipaswa kukamilisha muda wake wa kuhudumu tarehe mbili mwezi huu wa mei ameongezewa muda wa kuhudumu na rais William Ruto. Kupitia kwa gazeti rasmi la serikali , chesang aliteuliwa tarehe 7mei mwaka […]

MWANAFUNZI WA MKU AMEPATIKA AKIWA AMEUAWA HUKO THIKA

Makachero wa idara ya upelelezi DCI wanachunguza kisa ambapo Faith Musembi mwanafunzi mwenye umri wa miaka 19 katika chuo kikuu cha MKU amepatikana ameuliwa katika mtaa wa pilot Thika kaunti ya Kiambu. Inaarifiwa mwili wake uligunduliwa na babaye Bonface Musembi katika mtaa huo ulioko wadi ya hospital Thika. Kwa mujibu wa babake marehemu alipokea simu […]

KAUNTI YA KISUMU IMESITISHA MCHAKATO WA KUWAAJIRI WAHUDUMU WAPYA WA AFYA

Serikali ya kaunti ya Kisumu imesitisha mpango iliokuwa nao wa kuwaajiri wahudumu wa afya wakiwemo madaktari kwa kandarasi. Mwenyekiti wa chama cha madaktari KMPDU Dennis Miskela amesema kuwa amezungumza na gavana wa Kisumu Anyang Nyongo ambaye amesema hatua hiyo inafuatia kusitishwa kwa mgomo wa madaktariKaunti ya Kisumu ilikuwa imetangaza nafasi za mafiasa wa afya ambao […]

WACHANA NA WANAFUNZI

Shule zikitarajiwa kufunguliwa jumatatu wiki ijayo Waziri wa elimu Ezekiel Machogu amewaagiza walimu wakuu katika kaunti ya transnzoia kuwasilisha orodha ya majina ya walimu wakuu ambao wameongeza karo ya shule kinyume na muongozo wa wizara ya elimu ili waadhibiwe. Vile vile machogu amewaagiza walimu wakuu kutowatuma nyumbani wanafunzi kwa kukosa sare rasmi za shule na […]

NIMENAWA MIKONO

Vikao vya kusikiliza hoja ya kumwondoa afisini Waziri wa kilimo Mithika Linturi kutokana na Sakata ya mbolea ghushi vimekamilika leo hii. Mbunge wa Bumula Jack Wamboka ambaye ndiye aliyewasilisha hoja hiyo bungeni ameiomba kamati inayochunguza hoja hiyo kuhakikisha kwamba Linturi ameondolewa afisini. Akiwasilisha hoja yake ya mwisho mbele ya kamati hiyo inayoongozwa na mbunge maalum […]

TUWASHAURI WATOTO

Baadhi ya viongozi wa kidini wanaitaka serikali kupitia wizara ya elimu kuwapa ushauri nasaha wanafunzi ambao jamaa zao walifariki au kujeruhiwa katika janga la mafuriko. Mwenyekiti wa kanisa la Kenya Evangelical Alliance tawi la Nandi Teddy Kisivuli amesema ni vyema kwa wanafunzi na walimu kupewa ushauri nasaha ili kuepuka msongo wa mawazo hasa shule zinapofunguliwa […]

JENGO LA MAUTI BUNGOMA

Idadi ya watu isiyojulikana ingali imekwama kwenye vifusi baada ya kuangukiwa na jengo lililokuwa likibomolewa katika soko la kanduyi kaunti ya bungoma. Jengo hilo limekuwa chini ya ubomozi wa kaunti hiyo kuanzia wikendi iliyopita kwa ajili ya upanuzi wa uwanja wa wa masinde muliro kwa matayarisho ya sherehe za madaraka. Waliofukiwa kwenye vifusi wanaripotiwa kuwa […]