KOCHA WA POLICE BULLETS ASHABIKIA LIGI YA WANAWAKE

Kocha mkuu wa Mabingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake ya Kenya, Kenya Police Bullets, Beldine Odemba anaamini kuwa timu ya taifa ya wanawake Harambee Starlets inaweza kufaidika kutokana na utaalam wa ligi za wanawake.  Odemba ametoa changamoto kwa Shirikisho la Soka la Kenya kupata udhamini wa ligi hiyo ili kurahisisha shughuli zake, jambo ambalo pia […]

KOCHA ODHIAMBO HAJARIDHISHWA NA MATOKE YA KIKOSI CHAKE

Kocha mkuu wa Equity Dumas Carrey Odhiambo hajafurahishwa na Mchezo wao katika msimu wa kawaida huku timu hiyo ikielekeza fikira zake kwa mchujo ambao utakamilika kwa uteuzi wa bingwa wa michuano ambayo inakuja. Kulingana na Odhiambo, Dumas hawakufanya vyema katika mechi kadhaa, hivyo basi kuporomosha pointi zao .           ` Wanabenki hao waliwazaba Ulinzi Warriors 61-57 […]

CHIFU AKAMATWA GARISSA KWA KUCHUKUA HONGO

Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) imemkamata chifu katika Kaunti ya Garissa kwa madai ya kuwaibia wakimbizi wanaotafuta huduma katika afisi yake. Katika taarifa EACC jana Jumanne ilisema kwamba Abdirahman Shafe Yussuf, Chifu wa eneo la Bulla Mzuri, amekuwa akidai hongo kutoka kwa wakimbizi katika mchakato unaoendelea wa kufuta alama za vidole kutoka […]

MAREKANI YATOA MSAADA WA SODO 860,00 KWA WANAFUNZI

Marekani imetoa msaada wa sodo elfu 860,000 kwa shule za msingi za umma za humu chini ya mpango wa Sanitary Towels Akipokea shehena hiyo katika Taasisi ya Ukuzaji Mtaala wa elimu nchini (KICD) jana Jumanne, Katibu Mkuu wa Elimu ya Msingi (PS) Belio Kipsang alishukuru ubalozi wa Marekani mjini Nairobi, USAID na Idara ya Ulinzi […]

ZAIDI YA WAKULIMA ELFU 35 KUNUFAIKA NA MPANGO WA BT COTTON

Zaidi ya wakulima elfu 35 katika kaunti ya Homabay wamepata afueni baada ya kupata mbegu za pamba zilizokuzwa kiteknolojia yaani BT COTTON tani elfu kumi ambazo ziligharimu shilingi 72. Wakulima hao wamepewa mbegu hizo kama hatua ya kufufua klilimo cha pamba katika kaunti hiyo. Gavana wa Homabay Gladys Wanga na naibu wake Oyugi Magwanga wameongoza […]

UCHAGUZI WA KTDA NYAMIRA

Wakulima wa zao la majani chai katika kaunti ya Nyamira wameshauriwa kuwa makini na wale watakao wachagua kuwaongoza Kampeni za kuwachagua wakurugenzi wa almashauri ya maendeleo ma majani chai nchini KTDA. Katika kikao na wanahabari katika kituo cha ukusanyaji na upimaji zao la chai eneo la Bomondo Nyamira mjini baadhi ya wakulima hao wamewashauri wakaazi […]

KAUNTI KUPOKEA ZAIDI YA BILIONI 400 KWA MARA YA KWANZA

Kwa mara ya kwanza katika makadirio ya bajeti, serikali za kaunti zitapata zaidi ya shilingi bilioni 400, huku mwenyeketi wa kamati ya bajeti katika bunge la kitaifa Ndindi Nyoro akisema mgao wa kaunti katika mwaka wa kifedha ujao ni shilingi bilioni 400.1 Kwa mujibu wa Nyoro, mvutano uliokuwepo baina ya bunge la kitaifa na seneti […]

UFARANSA, NAKURU KUSHIRIKIANA KUIMARISHA MAENDELEO

Balozi wa ufaransa humu nchini Arnaud Suquet serikali ya Ufaransa itashirikiana na serikali ya kaunti ya Nakuru kuimarisha sekta kama vile utalii, kilimo biashara, uwezeshaji wa wanawake na maendeleo ya teknologia ya habari na mawasiliano. Akiwa kwenye ziara ya kaunti hiyo, Suquet ameitaja kaunti ya Nakuru kama kitovu cha kilimo katika kanda hiyo ya bonde […]

UNYANYAPAA, UBAGUZI WAIPONZA SHULE

Jopo la majaji watano linaloshughulikia ubaguzi dhidi ya waathiriwa wa ugonjwa wa UKIMWI limeiagiza shule ya msingi ya Najah iliyoko katika kaunti ya Garissa kumfidia mwanamke mmoja shilingi elfu 650 kutokana na unyanyapaa na ubaguzi aliofanyiwa mwanawe aliye na virusi vya UKIWMI. Jopo hilo linaloongozwa na Caroline Mboku, limetoa uamuzi huo baada ya kubainika kwamba […]

WAFUNGWA KWENYE KESI YA THUO KUHUKUMIWA JUNI

Wafungwa sita waliopatikana na hatia ya mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Juja George Thuo watahukumiwa tarehe 21 mwezi ujao, huku mjane wa marehemu Judy Thuo akiiomba mahakama kuwapa adhabu kali. Jaji Roselyn Korir amesema atatoa uamuzi wake kuhusu hukumu ambayo iataashiria kukamilika kwa kesi ya mauaji ya Thuo Wafungwa hao ni Paul Wainaina Boiyo, msaidizi […]