MWANAMKE AZUILIWA JUJA KWA KUMCHOMA KISU MPENZI WAKE

Polisi huko Juja wanamzuilia Cynthia Nakato, mwenye umri wa miaka 20, kwa madai ya kumchoma kisu mara saba mpenzi wake Peter Macharia, 23, na kusababisha kifo chake katika eneo la Mastore, Juja, Januari 20, 2024. Mwili wa marehemu umepelekwa katika chumba cha maiti kwa uchunguzi wa baada ya kifo, huku polisi wakisema uchunguzi unaendelea. Kamanda […]

HUDUMA KENYA YATAKIWA KUPIGA JEKI MIRADI YA SERIKALI

Idara ya huduma Kenya imetakiwa kupiga jeki juhudi za serikali kuhakikisha kuwa wakenya Zaidi wanajisajili kwenye bima ya Taifa Care. Akizungumza kwenye kongamano la mameneja vituo vya Huduma Center jijini Mombasa, katibu katika wizara ya utumishi wa umma Amos Gathecha ameitaka idara hiyo pia kuorodhesha idadi ya wakenya waliosajiliwa kupitia huduma Kenya. Aidha, ametoa hakikisho […]

SIWALIPI, GAVANA LUSAKA KWA WANAKANDARASI

Wanakandarasi wanaojenga madarasa ya chekechea kwenye kaunti ya Bungoma wameonywa dhidi ya kufanya kazi duni kwenye ujenzi huo, hatua ambayo inahatarisha maisha ya wanafunzi. Akizungumza katika eneo bunge la Bumula, gavana wa Bungoma Ken Lusaka ameonya kuwa serikali yake italazimika kukosa kuwalipa wankandarasi wanaokosa kuafikia viwango hitajika vya ujenzi. Amezungumza wakati wa uzinduzi wa usambazaji […]

MGOMO: WAGONJWA WAILILIA SERIKALI

Wagonjwa katika hospitali za umma wameendelea kukosa huduma za matibabu kwa siku ya pili kutokana na mgomo wa maafisa wa kliniki, baadhi yao sasa wakiitaka serikali kuangazia malalamishi ya maafisa hao ili kuondoa mahangaiko hospitalini. Wakizungumza na wanabahari, baadhi ya wanaosaka matibabu wamesema kuwa migomo ya mara kwa mara miongoni mwa wahudumu wa afya imeathiri […]

WAKAZI WA MAGHARIBI WATOA UJUMBE WA RAIS RUTO

Ziara ya Rais William Ruto katika eneo la Magharibi mwa nchi imeendelea kwa siku ya pili huku wakazi wakimtaka Rais kutimiza ahadi zake kuhusu utekelezaji wa miradi eneo hilo. Baada ya kikao na viongozi wa eneo hilo kwenye Ikulu ndogo ya Kakamega, Rais anatarajiwa kuongoza uzinduzi wa mradi wa kusambaza umeme mashinani katika eneo bunge […]

SUSWA: IPOA YAAHIDI HAKI KWA WAATHIRIWA

Katika juhudi za kurejesha utulivu na mshikamano katika eneo la Suswa kaunti ya Narok, mamlaka ya kutathmini mienendo ya maafisa wa polisi IPOA imesema inafanya uchunguzi wa kina kwenye mauaji ya watu wawili eneo hilo mwishoni mwa juma lililopita. Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, haki itapatikana kwa waathiriwa baada ya uchunguzi kukamilika kwenye machafuko hayo […]

WAFANYAKAZI WA MRADI WA NYUMBA WAGOMA BUSIA

Shughuli za ujenzi katika mradi wa serikali wa makazi ya bei nafuu katika eneo la Alema, eneo bunge la Funyula kaunti ya Busia zimekwama baada ya wafanyakazi kwenye mradi huo kugoma, wakimlaumu msimamizi kwa madai ya kutowasilisha matozo yao ya bima ya SHA na NSSF kwa afisi husika. Wakizungumza na wanahabari baada ya kususia kazi, […]

ABAUTANI YA WAFUGAJI KAJIADO KUHUSU CHANJO

Mpango wa serikali kuwapa chanjo mifugo humu nchini umepigwa jeki baada ya wafugaji katika kaunti ya Kajiado waliokuwa wamepinga mpango huo kubadili msimamo na kusema wataruhusu mifugo wao kuchanjwa. Wakizungumza kwenye kikao cha kuwahamasisha wafugajki katika eneo la Kimana Kajiado Kusini, wafugaji hao wamechukua uamuzi huo baada ya kupata ufahamu wa kutosha kuhusu mpango huo. […]

“TUOKOLEE NZOIA YETU” GAVANA LUSAKA

Katika juhudi za kuhakikisha wakulima wa miwa katika kiwanda cha sukari cha Nzoia wanaboresha Maisha yao, gavana wa Bungoma Ken Lusaka amemwomba Rais William Ruto kuingilia kati na kutatua matatizo ya kifedha kwenye kiwanda hicho. Akizungumza katika eneo la Mumias kaunti ya Kakamega ambako Rais amezindua bonasi kwa wakulima wa miwa, Lusaka amekariri haja ya […]

WATU WATANO WAFARIKI KATIKA AJALI HUKO MIGORI

Uchunguzi umeanzishwa na maafisa wa polisi baada ya watu watano, wakiwemo walimu wawili, kufariki papo hapo baada ya ajali iliyohusisha lori na pikipiki mbili katika daraja la Nyametembe, Kaunti ya Migori, usiku wa kuamkia leo Mashuhuda wanasema lori lililokuwa likiendeshwa kwa kasi lilipoteza mwelekeo na kugonga waendesha pikipiki wawili waliokuwa na abiria, na kuwaua wote […]