MASHARTI MAPYA KWA WALIMU WATARAJIWA

Tume ya kuwaajiri walimu TSC imetoa mapendekezo mapya kwa wanaolenga kusomea kozi za ualimu katika vyuo vikuu na taasisi za mafunzo ya ualimu, ikipendekeza kwamba anayetaka kufundisha katika shule za sekondari ya juu na sekondari msingi ni sharti awe na alama ya B+ na zaidi katika masomo mawili anayotaka kufunza. Kupitia taarifa, TSC imesema kwamba […]

EACC YAPATA MKUU MPYA

Wakenya wanatarajia huduma zilizoimarika kutoka kwa tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC baada ya Abdi Ahmed Mohamoud kuapishwa rasmi kuwa afisa mkuu mtendaji wa tume hiyo kuhudumu kwa miaka 6 na kujaza nafasi ya Twalib Mbaraka aliyestaafu. Mohamoud ameapishwa na jaji mkuu Martha Koome, akiahidi kuimarisha utendakazi wa tume hiyo na kupambana na […]

KINDIKI: SERIKALI KUZINDUA MAENEO YA BIASHARA KILA KAUNTI

Huenda shughuli za kibiashara na kilimo zikaimarika kote nchini iwapo serikali kuu itatimiza ahadi yake ya kuzindua kati ya maeneo 6-10 ya biashara na uzalishaji katika kaunti zote 47 kufikia mwisho wa mwaka huu. Akizungumza katika kikao na magavana 19 kutoka kaunti 19 ambazo zimeorodheshwa kwa ujenzi wa maeneo maalum`ya biashara katika awamu ya kwanza […]

WAUGUZI BUNGOMA WAANZA MGOMO, WAWATAKA WAGONJWA WAONDOKE

Baadhi ya wakazi katika kaunti ya Bungoma wametatizika kupata huduma za kimatibabu katika vituo vya umma kwenye kaunti hiyo kufuatia mgomo wa wauguzi wanaolalamikia madai ya kutotekelezwa kwa mkataba wao. Wakizungumza mjini Bungoma, wauguzi hao wamelalamikia mazingira duni ya kazi, wakishikilia kwamba hawatarejea kazini hadi malalamishi yao yatakapoangaziwa. Miongoni mwa matakwa yao ni ajira ya […]

MHUDUMU WA MPESA APIGWA RISASI KATIKA TUKIO LA UHALIFU MUKURWEINI NYERI

Polisi wanaendelea kuwasaka watu waliompiga risasi Mhudumu wa Mpesa na kujeruhiwa katika tukio la wizi katika Mji wa Kiahungu, Kaunti ya Nyeri. Kulingana na polisi, mwanamke huyo alikuwa akirejea nyumbani baada ya shughuli za siku, akiwa na mwenzake, walipovamiwa na wanaume wawili, mmoja akiwa na bastola. Wahalifu walimnyang’anya KSh.160,000 taslimu, simu tatu, na bidhaa mbalimbali […]

WAZAZI WASHAURIWA KUTHIBITI MATUMIZI YA MITANDAO KWA VIJANA

Wito umetolewa kwa wazazi kuwashauri wanao kuhusi mathara yanayoweza kutokana na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii. Kiranja wa wachache katika bunge la kitaifa Milly Odhiambo amewakosoa vijana kufuatia matumizi mabaya ya kijamii kwa kuwashambulia viongozi mitandaoni. Vile vile amekashifu matukio ya hivi majuzi ambapo wakenya wanaokosoa serikali mitandaoni wamekuwa wakitekwa nyara kiholela bila hatua […]

MARY MUTHONI; HAKUNA HMPV KENYA

Wakenya wamehakikishiwa kuwa wizara ya afya inafanya kila iwezalo kuthibiti maambukizi ya ugonjwa wa m-pox. Wizara ya afya aidha imesema kuwa imeimarisha uchunguzi wa HMPV na mpox katika mipaka yote ya kenya. Kwa mujib u wa katibu wa afya ya umma Mary Muthoni serikali imeimarisha uchunguzi wa watu wote wanaokuja humu nchini na kwamba kenya […]

MAN UNITED WAICHARAZA ASENALI 5-3

Wachezaji kumi wa Manchester United waliwalaza Arsenal 5-3 kwa penalti baada ya sare ya 1-1 katika raundi ya tatu ya Kombe la FA. United walilipiza kisasi kufuatia kichapo cha 2-0 kutoka kwa Arsenal kwenye Ligi Kuu mwezi Desemba. Bruno Fernandes aliwaweka United kifua mbele kwa shuti kali dakika ya 52, lakini Diogo Dalot alitolewa nje […]

NAIVAS WAILAZA MSA 4-1 NYUMBANI

Robert Karisa alifunga mabao mawili huku Naivas FC wakiwafunga Mombasa Stars 4-1 kwenye mechi ya Ligi ya Kitaifa ya Daraja la Kwanza (NSL) iliyochezwa Serani, Mombasa. Newton Ochieng na Markvivan Kesa waliongeza mabao mengine kwa Naivas, huku Gabriel Michael akifungia Stars bao la kufutia machozi. Ochieng alifunga bao la kwanza dakika ya 45 kwa shuti […]