MAAFISA WA KLINIKI WAILAUMU SERIKALI KWA KUEPUKA MASUALA YAO WAKATI MGOMO WA KITAIFA UKIENDELEA

Shirikisho la Maafisa wa Kliniki la Kenya (KUCO) limelaani serikali kwa kutumia nguvu kupita kiasi huku mgomo wao ukiendelea. KUCO inadai serikali imeshindwa kushughulikia masuala yao, kama vile ubaguzi wa Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA) na kukataa kutoa nafasi kwa vituo vya afya vinavyomilikiwa na maafisa wa kliniki. Maafisa wa kliniki wametoa notisi ya […]

CITY YARUDI KATIKA KIWANGO BORA BAADA YA USHINDI WA 6-0 DHIDI YA IPSWICH

Manchester City ilishinda 6-0 dhidi ya Ipswich, huku Phil Foden akifunga mabao mawili na Mateo Kovacic akifunga bao la kuvutia. Jeremy Doku, Erling Haaland, na James McAtee waliongeza mabao baada ya mapumziko, ikifanya City kushinda kwa kishindo. Huu ni ushindi wa tatu kwa City katika mechi zao nne za ligi, wakiwa na matumaini ya kurejea […]

MANCHESTER UNITED WALAZWA MABAO 3-1 NA BRIGHTON

Manchester United walizabwa mabao 3-1 na Brighton kwenye Uwanja wa Old Trafford, wakati wakimkumbuka gwiji wa klabu Denis Law, aliyefariki Ijumaa akiwa na miaka 84. Yankuba Minteh alifunga bao la mapema kwa Brighton kabla ya Bruno Fernandes kusawazisha kupitia penalti. Kaoru Mitoma na Georginio Rutter walifunga mabao mengine, wakiiwezesha Brighton kupanda hadi nafasi ya tisa, […]

SOKA YA KENYA YAOMBOLEZA KIFO CHA MWENYEKITI WA MATHARE UNITED BOB MUNRO

Mkurugenzi Mtendaji wa Mathare United, Jacktone Obure, amethibitisha kifo Bob Munro mtaalamu wa soka ambaye alifariki asubuhi ya jana Jumapili nyumbani kwake huko Westlands, Nairobi. Munro anahusishwa na kuongoza moja ya mashirika makubwa ya soka nchini Kenya, ambalo limetengeneza mamia ya wachezaji bora wa soka. Mnamo Disemba 12, 2024, wakati wa sherehe za Siku ya […]

MCF FC YAIBWAGA MOMBASA UNITED 3-0 KATIKA MECHI YA NSL

MCF FC iliifunga Mombasa United mabao 3-0 katika mechi ya Ligi ya Kitaifa Daraja la Pili (NSL) kwenye Uwanja wa Serani, Mombasa. Mabao ya MCF yalifungwa na James Olweny, John Okoth, na John Ochieng. Olweny alifunga bao la kwanza dakika ya 30 baada ya pasi safi kutoka kwa Ezekiel Okare. Okoth aliongeza la pili dakika […]

KAGWE AAHIDI KILIMO ‘SAFI’ KWA VIJANA

Wengi wa vijana nchini hawajihusishi na kilimo kutokana na mbinu zisizo na mvuto zinazotumika, nami nitahakikisha sekta hiyo inarekebishwa. Ndiyo kauli ya waziri mteule wa kilimo Mutahi Kagwe, akizungumza alipofika mbele ya kamati ya uteuzi katika bunge la kitaifa kueleza ufaafu wake wa kuhudumu kwenye wadhifa huo. Amesema kuwa iwapo ataidhinishwa, atashirikiana na wizara nyingine […]

MATOKEO NI YA WALIMU, SI WANAFUNZI- WAKAZI BUSIA

Wakazi wa Bumala kaunti ya Busia wamefanya maandamano kulalamikia matokeo duni yaliyorekodiwa na watahiniwa wa mtihani wa KCSE katika shule ya Bumala B, wakiulaumu usimamizi wa shule hiyo kwa matokeo hayo. Wakizungumza baada ya maandamano, wakazi hao wameshinikiza mageuzi katika usimamizi wa shule hiyo. Kwenye mtihani huo, shule hiyo ilipata alama ya wastani ya 3.23, […]

NAIROBI YAZIDI KUDHIBITI USAFI WA JIJI KWA MATATU NA WAFANYABIASHARA WADOGO

Serikali ya Kaunti ya Nairobi imetoa miongozo kwa wamiliki wa matatu kufuatia wasiwasi kuhusu shughuli zinazodaiwa kuzuia shughuli za usafi katikati ya jiji. Geoffrey Mosiria, Afisa Mkuu wa Mazingira wa Kaunti, katika taarifa ameeleza kwamba maeneo mengi ya matatu yanabaki yakikaliwa na magari usiku, yakizuia shughuli za usafi. Kama matokeo, alielekeza kwamba magari yote yaondoke […]

AFUENI YA NG-CDF KHWISERO

Ni afueni kwa wakazi wa eneo bunge la Khwisero kaunti ya Kakamega baada ya hazina ya ustawishaji wa eneo bunge hilo NG-CDF kutenga kima cha shilingi milioni 35 kugharamia karo ya wanafunzi wa shule za kutwa. Mbunge wa eneo hilo Christopher Aseka amesema kuwa tayari shilingi milioni 8 zimetengwa kufanikisha mpango huo kwa awamu ya […]

TUMEMSAMEHE MUUAJI, FAMILIA YA IAN

Tumemsamehe yeyote aliyehusika katika mauaji ya mtoto wetu, na hatutashinikiza kujua aliyehusika. Ndiyo kauli ya familia ya Ian Sing’oei ambaye mwili wake ulipatikana katika eneo la Mwiki jijini Nairobi Jumamosi iliyopita, familia hiyo ikizungumza wakati wa mazishi ya kijana huyo. Babake Ian, John Korir ambaye ni kamishna wa kaunti ya Elgeyo Marakwet na mamake ambaye […]