MUGIRANGO: WIZARA YA AFYA YACHUNGUZA UGONJWA ‘MGENI’

Huku waathiriwa Zaidi wakiendelea kulazwa hospitalini kutokana na ugonjwa usiojulikana katika eneo la South Mugirango kaunti ya Kisii, wizara ya afya imeendeleza uchunguzi dhidi ya ugonjwa huo ambao hadi sasa umeaathiri zaidi ya watu 200. Kulingana na katibu katika wizara hiyo Mary Muthoni, sampuli zimekusanywa kutoka kwa wagonjwa na watu waliotangamana na wagonjwa, akiwahimiza wakazi […]

ATI ATI ZA SHA

Hisia mbali zimeendelea kutolewa kuhusiana na changamoto zinazokabili sekta ya afya, serikali sasa ikitakiwa kuchukulia suala hilo kwa uzito na kuhakikisha wakenya wanapata huduma zilizo bora za afya. Katika mahojiano na runinga moja nchini mapema leo, mbunge wa Dagoreti North Beatrice Elachi, ameibua hofu kuhusu uwezekano wa maafisa katika wizara ya afya kuhujumiana, naye mwenzake […]

SERIKALI NJIANI KUBUNI AJIRA, KINDIKI

Kama njia mojawapo ya kubuni nafasi nyingi za ajira kwa wakenya na kuimarisha uchumi wa nchi, serikali imesema inatoa kipaumbele kwa ufufuzi wa sekta za kilimo na mifugo, ikiwa ni mojawapo ya ajenda yake ya kubadilisha uchumi. Haya ni kwa mujibu wa naibu rais Kithure Kindiki, akisema tayari serikali imepiga hatua katika kuanzisha vituo vya […]

NCIC YAMTAKA GACHAGUA AKOMESHE “UCHOCHEZI”

Huku taifa likiendelea kushuhudia joto la kisiasa, tume ya uwiano na utangamano NCIC imemwonya aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua dhidi ya kutoa matamshi ambayo tume hiyo imeyataja kuwa ya chuki na yanayoweza kuleta uhasama nchini. Kupitia taarifa ya mwenyekiti wake Samuel Kobia, tume hiyo imenukuu baadhi ya matukio ya Gachagua ikiwemo matamshi yake aliyotoa katika […]

MTEGO WA STIMA PLAZA: WAWILI WAFUTWA KAZI

Maafisa wawili wakuu katika serikali ya kaunti ya Nairobi wamesimamishwa kazi wakidaiwa kutoa maagizo kwa madereva wa malori ya kuzoa taka kutupa taka nje ya jengo la Stima Plaza wakati wa mzozo baina ya serikali hiyo na kampuni ya Kenya Power. Haya ni kwa mujibu wa gavana Johnson Sakaja, ambaye amezungumza akiwa mbele ya kamati […]

WAITITU ANYIMWA DHAMANA NA MAHAKAMA

Ni pigo kwa gavana wa zamani wa Kiambu Ferdinand Waititu baada ya ombi lake la kutaka aachiwe huru kwa dhamana akisubiri rufaa yake ya kupinga hukumu dhidi yake kutupiliwa mbali kwa misingi kwamba hajawasilisha sababu za kuishawishi mahakama impe dhamana hiyo. Miongoni mwa sababu alizotoa kutaka dhamana ni kuhusu afya yake, sababu ambayo mahakama imepinga […]

HISIA ZA SHA

Licha ya Rais William Ruto kukiri kuwepo kwa changamoto katika utoaji huduma za matibabu chini ya bima ya SHA, baadhi ya wandani wake wameendelea kutetea bima hiyo wanayosisitiza kuwa inafanya kazi ipasavyo. Katika mahojiano na runinga moja nchini mapema leo, seneta wa Bomet Hillary Sigei ameitetea bima hiyo, hatua ambayo imepingwa vikali na mwenzake wa […]

HATUTIKISIKI, KINDIKI AAPA KUHUSU MIRADI YA SERIKALI

Licha ya ukosoaji mkali dhidi ya baadhi ya sera na miradi ya serikali, naibu rais Kithure Kindiki amesema kuwa serikali ya Kenya Kwanza ipo tayari kufanya maamuzi magumu kuhusiana na utekelezaji wa miradi na sera zake. Kwenye kikao na wakenya wanaoishi nchini Namibia, Kindiki amesema serikali imejitolea kuimarisha sekta muhimu ili kufufua uchumi ambao umedorora […]