SALAH KUONDOKA LIVERPOOL WIKI HII

Fowadi wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri Mohammed Salah ameratibiwa kuelekea nchini Morocco atakapoongoza taifa lake katika fainali za taifa bingwa barani Afrika AFCON huku giza likigubika mustakabali wake katika klabu hiyo. Salah ambaye amegonga vichwa vya habari baada ya kulalamika hadharani kuhusu hali yake kwenye klabu ya Liverpool, aliingia kama nguvu mpya […]

KENYA YAAZIMIA KUIZAMISHA SENEGAL UFUKWENI

Kikosi cha mchezo wa handiboli ya ufukweni yaani beach handball cha wasichana chenye wachezaji wa umri wa miaka 17 kimeapa kulipiza kisasi dhidi ya mahasimu wao wa jadi Senegal iwapo watakutana kwenye fainali ya michezo ya 2025 African Youth Games hapo kesho. Kikosi hicho kinachonolewa na Evans Owino kilipoteza mikononi mwa Senegal hapo jana katika […]

MBEUMO ABEBE MZIGO WA UFUNGAJI NA UNAHODHA KWA CAMEROONAFCON 2025

Nyota wa Manchester United Bryan Mbeumo anakabiliwa na jukumu zito la kufunga mabaona kuongoza kikosi cha Cameroon katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika(AFCON) 2025 itakayochezwa Morocco mwezi huu. Baada ya mshambuliaji mkongwe Vincent Aboubakar kuachwa kwa mshangao, mzigo wakufunga mabao sasa umeangukia Mbeumo mwenye umri wa miaka 26, aliyejiunga naManchester United kutoka Brentford […]

AMBANI AONA NAFASI YA UBINGWA BAADA YA SARE NA KENYA POLICE

Kocha wa AFC Leopards Fred Ambani amesema anaamini timu yake inaweza kuwaniaubingwa wa FKF Premier League msimu huu, kufuatia sare tasa waliyopata dhidi ya KenyaPolice Jumamosi. Ambani aliwasifu wachezaji wake kwa kuonyesha kiwango cha juu tena, akisema matokeohayo ni ishara tosha kuwa Leopards wana uwezo wa kuendeleza mbio za kuwania taji ambalolimekuwa gumu kulipata kwa […]

OKAKA ASIFIA MPANGO WA NDONDI MASHINANI BAADA YA KENYAKUNG’ARA DUBAI

Bondia wa Kenya Defence Forces Robert Okaka ameusifu mpango wa Ndondi Mashinanikwa mchango wake mkubwa katika mafanikio ya timu ya taifa ya ndondi katika Mashindanoya Dunia ya Elite World Boxing Championships) yaliyofanyika Dubai, akielezea kiwangocha jumla kuwa cha kuridhisha zaidi ya wastani. Mpango huo wa kukuza vipaji mashinani ulioanzishwa mwaka 2019 umeelezwa kuwa nguzomuhimu iliyoiwezesha […]

KCB RFC YALENGA KOMBE LA ENTERPRISE CHINI YA MFUMO MPYA

Msimu huu wa Enterprise Cup umeanzishwa kwa mfumo mpya, ambapo timu nne za Kenyazitakazofuzu kutoka robo fainali za ndani zitakutana na timu nne za Uganda katika hatua yarobo fainali za kuvuka mipaka, hatua ambayo kocha anasema itawapa wachezaji uzoefumpya.Msaidizi wa kocha wa KCB RFC, Andrew Amonde, amesema wako tayari kushinda taji laEnterprise Cup msimu huu […]

KOOME: UMAKINIFU UTAPUNGUZA AJALI BARABARANI

Jaji mkuu Martha Koome amewataka wakenya kutotoa rushwa wanapopatikana na hatia za ukiukaji wa sheria za trafiki, akisema washikadau watafuatilia kwa karibu ukiukaji wa haki za kibinadamu wakati wa utekelezaji wa sheria za trafiki msimu huu wa Krisimasi. Akizungumza baada ya mkutano na wadau kwa lengo la kuimarisha utekelezaji wa sheria hizo, Koome amewahimiza wakenya […]

28 WAJERUHIWA KWENYE AJALI NAKURU

Watu 28 wanauguza majeraha, 12 kati yao wakiwa katika hali mahututi baada ya kuhusika kwenye ajali katika eneo la Salgaa kwenye barabara ya Nairobi- Nakuru mapema leo. Kulingana na shirika la Red Cross, basi hilo linalomilikiwa na kampuni ya Easy Coach lilikuwa likitoka Nairobi kuelekea Kisumu lilipogonga lori la kusafirisha mizigo na kusababisha ajali hiyo. […]

EPRA YATANGAZA BEI ZA MAFUTA KUSALIA ZILIVYO

Mamlaka ya kudhibiti wa kawi Petroli (EPRA) imetangaza kuwa bei za mafuta hazitabadilika kati ya tarehe 15 mwezi hu una januari 14. Kwa mwezi wa tatu mfululizo, mdhibiti ametangaza bei za pampu za rejareja za Super Petrol kuwa shilingi 184.52, Dizeli kuwa shilingi 171.47, na Mafuta ya Taa kuwa Ksh154.78, mtawalia, jijini Nairobi. Bei za hivi punde za pampu zinajumuisha […]

CITY MGONGONI PA ARSENAL EPL

Klabu ya Manchester City imeendelea kuwawekea shinikizo viongozi wa ligi kuu ya Uingereza Arsenal, baada ya kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Crystal Palace iliyokuwa imebashiriwa kuwa mechi ngumu kwa vijana hao wa Pep Guardiola. Hata hivyo, City walioponea mara kadhaa baada ya Yeremy Pino kupoteza nafasi za wazi, walishika mpini na kuelekeza makali […]