SARAH WAIRIMU ATAKA KESI YAKE IANZE UPYA

Mahakama kuu inatarajiwa kutoa uamuzi wake kuhusiana na Sarah Wairimu, mshukiwa mkuu wa mauaji ya mumewe raia wa Uholanzi Tob Cohen, anayetaka iagize kesi ya mauaji dhidi yake inayoendelea katika mahakama kuu za Kibra ifutiliwe mbali na kuanza kusikilizwa upya. Katika ombi lake, Wairimu anahoji kuwa vikao vya kesi hiyo vimekumbwa na dosari mbali na […]

WAKENYA 398 WAFARIKI KWENYE AJALI- TAKWIMU

Jumla ya wakenya 398 waliaga dunia kupitia ajali za barabara kati ya tarehe 1 hadi tarehe 30 mwezi huu pekee, hofu ikiibuka kuhusu visa vya ajali nchini. Kulingana na afisa wa mashauriano katika kitengo cha Trafiki kaunti ya Nairobi Boniface Otieno akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, visa hivyo ni ongezeko la asilimia […]

HALI YA KIWANGO CHA MPITO WA GRADE 10

Asilimia 98 ya wanafunzi wa gredi ya 9 mwaka jana imejiunga na gredi ya 10 kufikia sasa, serikali ikisema juhudi zinaendelea ili kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wameripoti shuleni. Haya ni kwa mujibu wa Waziri wa elimu Julius Ogamba, akisema ongezeko la kusajiliwa kwa wanafunzi hao limetokana na agizo la Rais William Ruto la kuwataka wanafunzi […]

HAZINA YATAKA BUNGE KUFUNGUA FEDHA ZA UWEKEZAJI

Hazina ya Kitaifa imetetea hali ya uchumi wa Kenya na kutaka Bunge liende kwa kasi katika kuidhinisha vyombo muhimu vya kifedha vinavyokusudiwa kufungua fedha kuu za uwekezaji. Kupitia taarifa  kwenye mtandao X hapo jana, Hazina imesema viashiria vya hivi karibuni vya uchumi vinaonyesha utulivu unaokua, hata wakati ambao wabunge wanajadili mwelekeo wa kifedha wa nchi. Ni swala ambalo liliibuka wakati wa mkutano […]

PSG, REAL MADRID WASUBIRI DROO YA UEFA CL

Mabingwa watetezi wa dimba la klabu bingwa bara Ulaya PSG na miamba wa soka barani humo Real Madrid, ni miongoni mwa miamba wa soka duniani wanaosubiri kwa hamu kufahamu wapinzani wake katika mechi za mwondoano wa kutinga awamu ya timu 16 za mwisho za dimba hilo. Droo hiyo itaandaliwa hii leo, baada ya awamu ya […]

NAIBOIS KUANZA UTETEZI DHIDI LA L15 FC

Mabingwa watetezi wa taji la FKF Kenya Cup, Nairobi United, wataanza kampeni ya kutetea taji hilo dhidi ya L15 FC, inayoshiriki ligi la FKF kiwango cha kaunti ya Kilifi katika raundi ya timu 64 inayojumuisha timu kutoka ligii kuu hadi zile za mashinani. Naibois, jinsi wanavyofahamika, waliwabandua miamba wa soka nchini Gor Mahia kutwaa taji […]

SAWE KUTETEA UBINGWA WAKE LONDON

Bingwa mtetezi wa mbio za London Marathon Sabastian Sawe, ameratibiwa kutetea ubingwa wake katika mbio zitakazoandaliwa tarehe 26 Aprili, akiamini kuwa huenda akahitaji kuvunja rekodi aliyoandikisha ili atetee ubingwa wake kutokana na ushindani mkali. Mkenya huyo mwenye umri wa miaka 29, anatarajia ushindani kutoka kwa vigogo wenza akiwemo Jacob Kiplimo wa Uganda aliyemaliza wa pili […]

RUTO AWATAKA VIJANA KUKUMBATIA NYOTA

Rais William Ruto amewahimiza vijana kote nchini kukumbatia mipango ya ujasiriamali inayoendeshwa na serikali kama vile mradi wa NYOTA, kama njia mojawapo ya kuimarika kiuchumi. Akizungumza mjini Kisii wakati wa uzinduzi wa mradi huo kwa vijana kutoka kaunti ya Kisii, Migori na Nyamira , Rais Ruto amesema mradi huo ni sehemu ya ahadi zilizotolewa na […]

UCHUNGU WA SUKARI NCHINI

Imebainika kuwa serikali haijalipa deni la zaidi ya shilingi bilioni 10 kwa wafanyakazi wa viwanda vya sukari nchini, licha ya kutangaza mageuzi ya kuboresha sekta hiyo wakati wa kukodisha baadhi ya viwanda hivyo kwa wawekezaji wa kibinafsi. Hii ni kufuatia mgomo wa wafanyakazi 5,000 kutoka viwanda 4 ambavyo ni Chemelil, Nzoia, Muhoroni na Sony kuanza […]

MLIPA USHURU KUGHARAMIA PENISHENI YA WABUNGE

Wakenya wanakabiliwa na uwezekano wa kuongezewa ushuru ili kugharamia malipo ya uzeeni ya wabunge iwapo mswada uliowasilishwa bungeni na mbunge wa Kitui Central Makali Mulu utapitishwa bungeni na kuwa sheria. Mswada huo unalenga masuala kadhaa ikiwemo kuwapa wabunge waliohudumu kwa muhula mmoja muda zaidi wa kulipa malipo yao ya penisheni waliopokea awali, huku wale waliohudumu […]