WAWILI WAKAMATWA KAWANGWARE KWA KUKIUKA SHERIA ZA KMPDC

Maafisa wa upelelezi DCI wamewakamata watu 2 kwa madai ya kuendesha kituo cha matibabu bila leseni mtaani Kawangware jijini Nairobi huku msako dhidi ya vituo bandia vya matibabu ukishika kasi. Washukiwa hao akiwemo mmiliki wa kituo hicho na mshirika wake, wamekamatwa mtaani Congo wakati wa msako unaoendeshwa na baraza la kudhibiti huduma za matibabu KMPDC. […]

WALALAMISHI WATAKA RUTO ATOLEWE JSC

Mswada umewasililishwa katika bunge la kitaifa ukilenga kuondolewa kwa aliyekuwa gavana wa Bomet Isaac Ruto kutoka wadhifa wa mwanachama wa tume ya huduma kwa mahakama JSC, kwa misingi kwamba amekuwa akijihusisha na siasa za miegemeo na hivyo kuhujumu uhuru na uadilifu wa mahakama. Walalamisshi kwenye mswada huo wanahoji kuwa uteuzi wake umesababisha kudorora kwa imani […]

KENYA, IMF KUANZA TENA MAZUNGUMZO FEBRUARI

Kenya inajiandaa kuanzisha upya mazungumzo na Shirika la Fedha la Kimataifa, IMF, mwezi Februari mwaka huu inapochunguza mpango mpya wa ufadhili, hay ani kwa mujibu wa maafisa katika Hazina ya Kitaifa. Mazungumzo hayo yalitarajiwa kuanza Januari lakini yaliahirishwa ili kuruhusu mashauriano zaidi ya ndani. Raphael Owino, ambaye ni msimamizi katika ofisi za Usimamizi wa Madeni ya Umma, amesema IMF inatarajiwa kurejea nchini […]

MIAMBA ULAYA KUPITIA NJIA NDEFU UEFA CL

Mabingwa watetezi wa ligi ya klabu bingwa bara Ulaya PSG watalazimika kushiriki mchujo yaani playoff baada ya kukosa nafasi ya moja kwa moja kuingia awamu ya 16 za mwisho, kufuatia sare ya bao 1-1 dhidi ya Newcastle United. PSG walimaliza katika nafasi ya 11, na iwapo wangepta ushindi wangeibandua Manchester City waliopata ushindi wa mabao […]

FURY KUREJEA ULINGONI APRILI DHIDI YA MAKHMUDOV

Bingwa wa zamani wa masumbwi katika kitengo cha heavyweight Tyson Fury, atamenyana na Arslanbek Makhmudov wa Urusi atakaporejea ulingoni mwezi Aprili baada ya kutangaza kurejea tangu kustaafu kwake. Pigano la raia huyo wa Uingereza na Mrusi Makhmudov anayeishi nchini Canada, litafanyika nchini Uingereza tarehe 11 mwezi Aprili, ingawa ukumbi haujatangazwa. Fury alistaafu kutoka mchezo wa […]

POLICE FC WASUASUA, TENA

Bao la pekee la Darius Msagha liliwapa wenyeji bandari ushindi mwembamba na muhimu dhidi ya bingwa mtetezi Police FC katika uga wa Mbaraki kaunti ya Mombasa kwenye mechi ya ligi kuu KPL hapo jana. Ushindi kwa vijana hao wanaonolewa na Bernard Mwalala unaendeleza rekodi ya kutopoteza mechi hadi 4, na wamepanda hadi nafasi ya 7 […]

“MAAFISA WA ELIMU HAWANA UFAHAMU”

Maswali yameibuka kuhusu maafisa wakuu wa wizara ya elimu akiwemo Waziri Julius Ogamba na makatibu wake kuendesha wizara hiyo ipasavyo, baada ya kuibuka kuwa hawana ufahamu kuhusu masuala ya kimsingi kwenye wizara hiyo ikiwemo gaharama ya kumwelimisha mwanafunzi mmoja. Wakiwa mbele ya wabunge, maafisa hao wameibua hofu kuhusu sera za elimu hasa mpito wa gredi […]

DUALE: SIWEZI KUJIUZULU!

Waziri wa afya Aden Duale amepuzilia mbali uwezekano wake kujiuzulu kuhusiana na madai ya kupotea kwa shilingi bilioni 11 katika bima ya afya ya jamii SHA, badala yake akitoa hakikisho kuwa wizara hiyo imeweka mikakati ya kuzuia wizi wa fedha. Katika mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Duale amekanusha madai ya kupotea kwa fedha hizo, […]

WAATHIRIWA WA BOMU 1998 WAPATA PIGO KORTINI

Inasubiriwa kuona iwapo waathiriwa wa mlipuko wa bomu mwaka wa 1998 jijini Nairobi watawasilisha kesi katika mahakama ya rufaa au la, baada ya mahakama kuu kutupilia mbali kesi yao ya kutaka wapewe fidia na hivyo kusitisha kesi ya kusaka haki kwa zaidi ya miaka 25. Katika uamuzi wake, jaji Lawrence Mugambi amesema walalamishi walishindwa kuthibitisha […]

UPINZANI WASISITIZA UMOJA, KUMTANGAZA NAHODHA

Muungano wa upinzani umesema kwamba uko katika hatua za mwisho za kumtangaza mgombea wake wa urais atakayemenyana na Rais William Ruto kwenye uchaguzi mkuu ujao, na utamweka wazi baada ya kongamano la kitaifa la wajumbe, NDC, la chama cha DCP chake aliyekuwa naibu Rais Rigathi Gachagua. Wakizungumza baada ya NDC ya chama cha DP chake […]