TRUMP: NITAIENDESHA VENEZUELA

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa serikali yake itamwelekeza kikamilifu cha kufanya kiongozi wa muda wa Venezuela Delcy Rodriguez, ukiwemo uuzaji wa mafuta kwa muda usiojulikana baada ya kumbandua Nicolas Maduro. Kauli ya Trump inajiri huku Delcy akina kwamba hakuna utawala wan je unaoeindesha Venezuela Hata hivyo, Trump amesema Marekani italiendesha taifa hilo la […]

WANAFUNZI TRANS MARA SOUTH SHULENI

Hatimaye wanafunzi katika shule ya Sitet Comprehensive eneo la Trans Mara South wamepata fursa ya kurejea shuleni kwa muhula wa kwanza baada ya maafisa wa usalama kuwaondoa watu waliokuwa wakiishi kwenye shule hiyo. Operesheni hiyo iliongozwa na chifu wa Olodonyo-Orok Paul Rutto, mkurugenzi wa elimu eneo hilo George Muchina akiripoti kuwa wanafunzi wapatao 250 waliripoti […]

DUALE, KUCO WAKOSA MWAFAKA

Huenda wakenya wakaendelea kuhangaika kupata matibabu kutokana na mgomo wa maafisa wa kliniki unaoendelea kutokana na mvutano kati ya viongozi wa muungano wa maafisa hao KUCO na Waziri wa afya Aden Duale, ambaye amedinda kutia saini mkataba wa maelewano ya kurejea kazini ulioidhinishwa na tume ya kuratibu mishahara ya wafanyakazi wa umma SRC. Kwa mujibu […]

UPINZANI WADAI NJAMA YA UDANGANYIFU 2027

Muungano wa upinzani umeibua madai ya kuwepo kwa njama ya kuiba kura kwenye uchaguzi mkuu ujao kupitia kampuni ya Smartmatic iliyotoa huduma za teknolojia kwenye vyombo vya dijitali vya uchaguzi wa mwaka wa 2022, ikitaka kandarasi ya kampuni hiyo ifutiliwe mbali. Kulingana na viongozi wa upinzani akiwemo kinara wa DCP Rigathi Gachagua, Kalonzo Musyoka wa […]

RUTO AWAPOTOSHA WAKENYA, MUSYOKA

Rais William Ruto analenga kutumia ajenda ya kuibadilisha Kenya kuwa mfano wa taifa la Singapore kuwapotosha wakenya na kuvuruga fikra zao ili wakose kumwajibisha kuhusiana na utendakazi wake. Haya ni kulingana na makamu wa zamani wa Rais Kalonzo Musyoka na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua, wakisema haifai kulinganisha Kenya na taifa jingine. Walikuwa wakizungumza kwenye […]

FATAKI ZA EPL

Manchester City watalenga kupunguza mwanya wa pointi kati yao na viongozi wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza Arsenal, watakapoikaribisha Brighton ugani Etihad leo usiku. City ambao walipoteza pointi 4 katika mechi 2 zilizopita, watakosa huduma za mabeki wao mahiri Ruben Diaz na Josko Gvardiol kutokana na majeraha, City wakilalizimika kumrejesha beki wao Max Alleyne […]

DIALLO ANG’AA KWA IVORY COAST

Kiungo wa Manchester United Amad Diallo alikuwa nyota mchezoni jana usiku wakati mabingwa watetezi wa dimba la taifa bingwa barani Afrika AFCON 2025 Ivory Coast waliwadhalilisha Burkina Faso kwa kibano cha mabao 3-0 kwenye awamu ya mwondoano, Ivory Coast wakiwa mabingwa watetezi wa kwanza wa AFCON kufika awamu ya robo fainali tangu mwaka wa 2010. […]

GOR YASHIKA USUKANI WA KPL

Mabingwa mara 21 wa ligi kuu ya soka KPL Gor Mahia, wamechukua uongozi wa ligi hiyo baada ya kuonyesha ubabe wao kwenye ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Kariobangi Sharks hapo jana. Ben Stanley alianzisha ufungaji katika dakika ya 20, kabla ya Ebenezer Adu-Kwaw kuongeza kabla ya kutamatika kwa kipindi cha kwanza. Sharks walitishia kuwapokonya […]

MATUMAINI YA KIKOSI CHA X-COUNTRY MAREKANI

Wanariadha wa Kenya watakaowakilisha taifa katika mashindano ya ubingwa wa Cross Country mwaka huu yatakayoandaliwa Jumamosi hii eneo la Tallahassee katika jimbo la Florida nchini Marekani wameelezea matumani ya kutetea ubingwa wa taifa kwenye mbio hizo. Licha ya mashindano hayo kutawaliwa na wanariadha binafsi wa Uganda, Kenya inajivunia ubingwa wa mbio hizo kwa jumla ulioandikishwa […]

MIGAWANYIKO YA KISIASA YAIBUKA

Tofauti za kisiasa zimeendelea kuibuka miongoni mwa vyama tanzu vya muungano wa upinzani na Kenya Kwanza, baadhi ya viongozi wakitangaza kugura vyama hivyo na kujiunga na vyama vinavyoegemea serikali ya Kenya Kwanza. Wa hivi punde ni naibu kinara wa chama cha DAP-K na naibu gavana wa Kakamega Ayub Savula, ambaye amegura chama hicho na kutangaza […]