MATAIFA YA AFRIKA MASHARIKI WASHIRIKI MCHUJO WA AFCON

Kenya, Uganda na Tanzania zitacheza mchujo wa kuwania kufuzu Fainali za kombe la Mataifa ya Afrika (CHAN) 2025 licha ya mataifa hayo matatu kuwa waandaji wenza wa michuano hiyo na wakiwa tayari wamehakikishiwa tiketi ya kushiriki. Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), mataifa hayo matatu yatacheza mechi za kufuzu kwa ukanda wa CECAFA, […]

HATUA ZA KIDHARURA ZICHUKULIWE

Waziri la Michezo Kipchumba Murkomen anataka hatua za haraka zichukuliwe ili kupanua uwakilishi wa Kenya katika Michezo ya Olimpiki kwa siku za usoni, akisisitiza haja ya kuzingatia michezo yenye kukosa uwakilishi kutoka Kenya na kuimarisha maandalizi ya mapema. Akizungumza katika warsha ya kimkakati ya Kamati ya Kitaifa ya Olimpiki ya Kenya (NOC-K) mjini Sagana, Murkomen […]

HUSSEIN ATAKA UCHAGUZI WA HURU NA HAKI

Huku uchaguzi unaosubiriwa kwa hamu na Shirikisho la Soka la Kenya FKF ukikaribia, Hussein Mohamed, mmoja wa wanaowania kiti cha urais, ametoa wito wa uchaguzi huru na wa haki. Akizungumza mjini Iten, Elgeyo Marakwet wakati wa fainali za kombe la Gavana wa Raia, Mohamed alisema kuzinduliwa kwa bodi ya uchaguzi kunafaa kuhakikisha kunaandaliwa uchaguzi wa […]

BRAD IBS AFURAHISHWA NA KIKOSI CHAKE

Kocha mkuu wa mabingwa wa Kitaifa wa Mpira wa Kikapu Ligi Kuu ya wanaume, Nairobi City Thunder, Brad Ibs, amefurahishwa na kikosi chake baada ya kupata ushindi wa kuongeza morali dhidi ya Kenya All Stars katika mechi ya kulirafiki wikendi. Thunder ambao walibeba taji hilo bila kupoteza mechi hata moja msimu uliopita, walipata ushindi wa […]

TER STEGEN

Kipa wa Barcelona, Marc-Andre ter Stegen atafanyiwa upasuaji wa mshipa wa goti uliochanika, huku nahodha huyo wa klabu hiyo akitarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa salio la msimu huu. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 32 alitolewa nje kwa machela baada ya kuanguka vibaya wakati timu yake iliposhinda 5-1 dhidi ya […]

LIPO TUMAINI HAITI, RAIS RUTO

Rais William Ruto ametoa wito kwa jamii ya kimataifa kuzidisha juhudi za kurejesha utulivu nchini Haiti, akikariri haja ya kuimarisha usalama na Maisha ya raia wa taifa hilo la Karibia. Akizungumza katika kongamano la viongozi kujadili mustakabali wa Haiti, Ruto amehimiza jamii hiyo kuisaidia Haiti kurejesha hali ya utulivu nchini humo. Aidha, Ruto ambaye maajuzi […]

WAKENYA WASHINIKIZA MSHIKAMANO, UMOJA

Wakenya kutoka matabaka mbali mbali wanaendelea kushinikiza mshikamano miongoni mwa viongozi ili kutuliza joto la kisiasa, ambalo wanahofia huenda likalemaza utendakazi wa serikali. Akizungumza kwenye kaunti ya Nyandarua, Waziri wa usalama wa kitaifa Kithure Kindiki amewahimiza viongozi kushirikiana kwa lengo la kuboresha Maisha ya wakenya. Wakati uo huo, wananchi wa kawaida wamesikitishwa na mirengo ambayo […]

ADANI: ONYONKA AIBUA ‘USHAHIDI’ MPYA

Mkataba baina ya serikali na kampuni ya Adani unaendelea kuchukua mkondo mpya kila kuchao, wakati huu seneta wa Kisii Richard Onyonka akiibua ushahidi mpya kwamba licha ya kampuni 3 kuwasilisha mapendekezo ya kuukarabati uwanja wa ndege wa kimataifa wa JKIA, mamlaka ya usimamizi wa viwanja vya ndege KAA ilipendelea kampuni ya Adani na kupuuza kampuni […]

GAVANA MUTAI AKODOLEA HOJA YA KUTIMULIWA

Huenda gavana wa kaunti ya Kericho Eric Mutai akabanduliwa kutoka mamlakani baada ya wawakilishi wadi kwenye kaunti hiyo kutishia kuwasilisha mswada wa kumbandua hii leo kutokana na madai ya utumizi pesa za umma na ukiukaji wa sheria. Wakiongozwa na kiongozi wa walio wengi katika bunge la kaunti hiyo Philip Rono, wawakilishi wadi hao wamelalamikia kupungua […]

WAWILI MAHAKAMANI KWA UFUJAJI WA FEDHA WEST POKOT

Maafisa wawili wa zamani katika serikali ya kaunti ya West Pokot wanatarajiwa kufikishwa katika mahakama jijini Eldoret kufunguliwa mashtaka ya ufujaji wa shilingi milioni 296 zilizokuwa zimetengewa hazina ya ufadhili wa masomo. Wawili hao waliokamatwa na tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC, walihojiwa hapo jana na kuzuiliwa kwenye kituo kikuu cha polisi jijini […]