APOSTLE MANYURU APINGA MSWADA ‘WA MUNGATANA’

Mwenyekiti wa muungano wa makanisa ya Pentecostal Voice of Kenya PVK ambaye pia ni kiongozi wa kanisa la Jesus Teaching Ministry Apostle Peter Manyuru, ameelezea hofu kuhusiana na mswada wa kudhibiti makanisa nchini, akisema mswada huo utalemaza shughuli za kanisa iwapo utapitishwa. Akizungumza na wanahabari jijini Nairobi akiwa ameandamana na viongozi wengine wa muungano huo, […]

GACHAGUA KIKAANGONI, MSWADA WA KUKOSA IMANI WAWASILISHWA

Seneta wa Tana River Danson Mungatana amewasilisha mswada katika bunge la seneti wa kutokuwa na imani na naibu rais Rigathi Gachagua kuhusiana na mienendo ya naibu huyo wa rais. Akiwahutubia wanahabari, Mungatana amesema kwamba Gachagua amekiuka sheria inayodhibiti mienendo ya naibu rais na utekelezwaji wa majukumu yake. Aidha, Mungatana amesema kuwa Gachagua amekuwa akitoa matamshi […]

WATAENDA WOTE, SENETA MAANZO

Mjadala wa kumbandua kutoka mamlakani naibu rais Rigathi Gachagua unaendelea kuchacha huku seneta wa Makueni Dan Maanzo akisema kwamba iwapo mswada huo utawasilishwa, mswada sawa na huo utawasilishwa dhidi ya Rais William Ruto. Akizungumza na wanahabari, Maanzo ameshikilia kwamba wawili hao walichanguliwa kwa tiketi moja na hivyo wanafaa kuondoka pamoja. Aidha, amesema kwamba Rais William […]

TUZUNGUMZIANE, GAVANA NDETI

Gavana wa Machakos Wavinya Ndeti ametoa wito kwa viongozi kuzungumziana badala ya kulumbana kwenye mikutano ya hadhara, akisema mienendo yao inatoa mfano mbaya kwa umma. Gavana huyo amewataka walio na tofauti za kisiasa kuheshimiana ili kudhibiti mihemko ya kisiasa miongoni mwa wananchi. Aidha, amesema majibizano kati ya naibu rais Rigathi Gachagua na wanaompinga hayaleti picha […]

KNUT YASHINIKIZA MASLHAI BORA KWA WALIMU WA BONI

Muungano wa walimu wa shule za msingi KNUT umeshinikiza serikali kuangazia na kutimiza matakwa ya walimu wanaofunza kwenye shule zilizo ndani ya msitu wa Boni. Walimu hao wanamtaka mwajiri wao TSC kuwapandisha vyeo na kuwapa marupurupu ya kufanya kazi katika mazingira magumu. Aidha, wamelalamikia kudhoofika kwa wenzao kiafya kutokana na mazingira magumu wanamofanyia kazi. Imetayarishwa […]

RUTO: UN IFANYIWE MAGEUZI KUZUIA MIGOGORO

Rais William Ruto ameshinikiza mageuzi katika baraza la usalama la umoja wa Mataifa ili kukabili changamoto zinazoibuka. Kwa mujibu wa Rais Ruto, mfumo uliopo kwa sasa umeshindwa kukabiliana na migogoro inayoibuka hususan suala la mabadiliko ya tabia nchi, kutokuwa na usawa na madeni. Akizungumza katika mkutano wa marais jijini New York ulioangazia mustakabali wa mataifa […]

POLISI WAWATAWANYA WAHADHIRI WANAOGOMA NAIROBI

Polisi jijini Nairobi wamewatanya kwa kuwarushia vitoza machozi wahadhiri waliokuwa wakiandamana wakilalamikia kutoketekelezwa kwa mkataba wao wa maelewano. Wahadhiri hao ambao wanapanga kuwasilisha hoja kwa bunge la kitaifa, wamekanusha madai ya Waziri wa elimu kwamba wameafikiana kurejea kazini, wakisema hawatatia Saini mkataba ambao unawabagua baadhi yao. Wakiongozwa na katibu mkuu wa UASU Constantine Wasonga, wahadhiri […]

MASAIBU YA GACHAGUA SI YA LEO, WAMUCHOMBA

Mbunge wa Githunguri Gathoni Wamuchomba ameibua madai mapya kuhusiana na masaibu ya kisiasa yanayomkumba naibu rais Rigathi Gachagua, akisema masaibu yake yalianza punde baada ya rais William Ruto kumteua Gachagua kuwa mgombea mwenza wake. Akizungumza kwenye mahojiano na runinga moja nchini mapema leo, Wamuchomba amesema baadhi ya vigogo wa mlima Kenya walimpendelea Waziri wa usalama […]

KENYA YAAHIDI KUWATUMA POLISI ZAIDI HAITI

Kenya imeahidi kuwatuma maafisa wengine 600 wa polisi katika taifa la Haiti wiki zijazo ili kushirikiana na wenzao waliotangulia katika kupambana na magenge ambayo yanadhibiti maeneo muhimu ya taifa hilo, likiwemo jiji kuu la Port-au-Prince. Idadi hiyo itafikisha jumla ya polisi 1,000 walioahidiwa kuwasilishwa nchini humo kusaidia kurejesha utulivu, kwa ushirikiano na vikosi kutoka mataifa […]

IEBC MPYA KUNGOJA ZAIDI KUTOKANA NA KESI

Uteuzi wa kamati ya kuwateua makamishna wapya wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC utakawia baada ya kesi mpya kuwasilishwa mahakamani ikipinga uamuzi wa jopo la kutatua migogoro ya kisiasa kumtangaza Augustus Kyalo Muli kuwa mwakilishi wa vyama vidogo vidogo katika kamati hiyo. Kesi hiyo iliyowasilishwa na Koki Muli, itatajwa Alhamisi wiki hii mbele […]