MWATSINGWA AIPA SS ASSAD USHINDI DHIDI YA MSA UNITED

SS Assad wamewashinda wenyeji Mombasa United, kwa bao 1-0 kwenye mechi ya Ligi ya Taifa Daraja la Pili (NSL) iliyochezwa jana Jumapili katika Uwanja wa Michezo wa Serani, Kaunti ya Mombasa. Hemed Mwatsingwa alifunga bao pekee la Assad katika dakika ya 15, kwa shuti la chini na kali lililomshinda mlinda lango wa Mombasa United, Kevin […]

JUBILEE YATAKA EACC KUCHUNGUZA ‘WASHIRIKA’ WA ADANI

Chama cha Jubilee kimeitaka tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC kuwachunguza na kuwakamata maafisa wa serikali wanaohusika na mkataba baina ya serikali na kampuni ya Adani, siku moja baada ya kuibuka kwamba kampuni hiyo inakabaliwa na mashtaka ya ufisadi nchini Marekani. Kupitia taarifa, katibu mkuu wa Jubilee Jeremiah Kioni amewataka maafisa wote husika […]

WAKENYA: HATUTAKI MASHIRIKIANO NA ADANI TENA

Wakenya wameibua hisia mseto kuhusiana na hatua ya rais William Ruto kufutilia mbali mkataba wa kibiashara na kampuni ya adani. Baadhi ya kina mama wametaja hatua hiyo kuwa ya kijasiri na ambayo imeonyesha ukomavu wa serikali kwa kuwa imebadilisha taswira ya serikali kwa kiwango kikubwa. Baadhi ya wakenya wameeleza kuwa hatua ya rais Ruto haijatokana […]

VIONGOZI WAMTAKA RAIS RUTO KUFUTILIA MBALI SHA

Viongozi mbali mbali wakiwemo wa kidini wameelezea kutorithishwa na utendakazi wa bima mpya ya jamii SHA. Kwa mujibu wa viongozi hao wagonjwa hasa wale wanaugua marathi sugu wanakabiliwa na changamoto kupata matibabu chini ya SHA. Viongozi hao aidha wamelalamikia hatua ya serikali ya kufanya madbadiliko ya bima ya afya b ila kutoa maelezo ya kina kwa umma. Imetayarishwa […]

KMA YATOA MAKATAA KWA SERIKALI KUTATUA MZOZO KUHUSU KODI YA LESENI ZA HOSPITALI

Muungano wa madaktari Kenya Medical Association umetoa makataa ya wiki mbili kwa baraza la mawaziri na serikali ya kitaifa ,kufanya mazungumzo na kutoa mwelekeo wa iwapo serikali zote za ugatuzi zitaendelea kuzitaka hosipitali kulipa kodi ya leseni ya kuhudumu ama la. Naibu wa rais wa muungao huo Dkt Ibrahimu Matende amesema kuwa baada ya wiki […]

KAUNTI ZAPUNGUZIWA MGAOMGAOKAUNTI ZAPUNGUZIWA MGAO

Huduma muhimu katika ngazi za kaunti zinatazamiwa kuathiriwa na hasara ya bilioni 13.5 zilizokuwa zimetengewa kauni za ugavi wa mapato. Kwa mujibu wa mwenyekiti wa baraza la magavana Ahmed Abdulahi serikali za kaunti zitatatizika kuafikia makubaliano muhimu ikiwa ni Pamoja na CBA ya madaktari iliyotiwa Saini nao baada yao kusitisha mgomo wao ikibainika kuwa fedha […]

RUTO AAGIZA KUSITISHWA KWA USHIRIKIANO NA ADANI

Wakenya waliokuwa wakipinga kukodishwa kwa uwanja wa ndege wa kimataifa wa JKIA kwa kampuni ya Adani wana kila sababu ya kutabasamu baada ya Rais William Ruto kuagiza kufutiliwa mbali kwa mikataba ya ushirikiano baina ya serikali na kampuni hiyo. Akizngumza katika majengo ya bunge wakati wa hotuba yake kwa taifa, Rais ameziagiza wizara za kawi […]

WAHADHIRI, SERIKALI WAKOSA MWAFAKA

Shughuli za masomo katika vyuo vikuu vya umma zimeendelea kuathirika kwa wiki ya 4 huku wahadhiri wakiitaka serikali iwape shilingi bilioni 9.7 za mishahara na marupurupu yao la sivyo waendelee na mgomo wao. Wakiongozwa na katibu wa muungano wa UASU Dakta Constantine Wasonga, wahadhiri wamesema mgomo ungalipo licha ya serikali kutoa shilingi bilioni 4.3. Hata […]

MMOJA AUAWA KIMILILI, NYUMBA ZABOLEWA

Hali ya kawaida imeanza kurejea katika kijiji cha Kibingei eneo bunge la Kimilili kaunti ya Bungoma baada ya polisi kuwakamata washukiwa watatu kufuatia mauaji ya mwanamme mwenye umri wa miaka 34 eneo hilo kuhusiana na kinachoaminika kuwa mzozo wa kimapenzi. Kwa mujibu wa kamanda wa polisi eneo la Kimilili Nzaka Mwitu, mwathiriwa kwa jina Ben […]

WAZIRI WANDAYI ATETEA ADANI LICHA YA TUHUMA

Waziri wa kawi Opiyo Wandayi ameitetea kampuni ya Adani mbele ya kamati ya kawi katika bunge la kitaifa akisema kandarasi ya serikali kwa kampuni hiyo haina dosari yoyote. Haya yamejiri wakati ambapo kampuni hiyo inakabiliwa na tuhuma za utoaji rushwa ili kupokea kandarasi ya kawi ya jua nchini India. Utata umeibuliwa kuhusu kandarasi ya kawi […]