WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA MBEGU HALALI

Katika juhudi za kuimarisha uzalishaji wa chakula nchini, wakulima wamehimizwa kutumia mbegu kutoka kwa kampuni zilizoidhinishwa na bodi ya udhibiti na ubora wa mbegu KEPHIS. Akizungumza katika kaunti ya Meru, mkurugenzi wa ubora wa mbegu nchini Simon Maina amesema kuwa serikali ina kesi 15 mahakani kuhusiana na mbegu ghushi, kesi 5 miongoni mwao zikiwa katika […]

WAJIBIKENI AMA MUENDE, RUTO AWAAMBIA MAAFISA

Wakenya wanatarajia huduma bora kutoka kwa serikali kuanzia sasa baada ya Rais William Ruto kuwaagiza mawaziri na makatibu wao watekeleze wajibu wao ipasavyo la sivyo wafutwe kazi. Akiwahutubia katika hafla ya kutia saini kandarasi ya utendakazi katika Ikulu ya Nairobi, Rais ametetea utendakazi wa serikali yake na kuahidi mageuzi Zaidi katika sekta kadhaa ikiwemo afya, […]

KANE ASISITIZA MSISIMUKO KWA KIKOSI CHAKE

Nahodha wa Uingereza Harry Kane anasema anacheza kwa kiwango chake cha juu zaidi kuwahi kutokea huku akipuuzilia mbali mapendekezo ya Kombe la Dunia la 2026. Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 31 alikiri kuwa alishtushwa na simu hiyo, lakini alifunga bao Jumapili katika ushindi wa 5-0 dhidi ya Jamhuri ya Ireland aliporejea kwenye kikosi cha […]

WACHEZAJI WATATU WA AFRIKA KUSINI WATEULIWA KWA TUZO

Mshambulizi wa Nigeria Ademola Lookman na mlinda mlango wa Afrika Kusini Ronwen Williams walikuwa miongoni mwa nyota watano walioteuliwa Jumatatu kuwania tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika wa Mwaka. Taarifa ya Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) imewataja beki wa Morocco, Achraf Hakimi, winga wa Ivory Coast, Simon Adingra na mshambuliaji wa Guinea, Serhou Guirassy […]

NZOIA SUGAR YALAMBA SUKARI YA USHINDI

Klabu ya Soka ya Nzoia Sugar ilipata ushindi mnono wa 1-0 dhidi ya Samwest Blackboots katika mpambano wa Ligi Kuu ya Kitaifa (NSL) uliofanyika jana jijini Nairobi. Ushindi huo, uliopatikana kwa bao kali la Ian Simiyu, ulileta ari inayohitajika sana na kuboresha kidogo msimamo wa ligi ya klabu. Kocha mkuu Charles Odero alitaja ushindi huo […]

HARAMBEE STARS IFANYIWE MABADILIKO

Nahodha wa zamani wa AFC Leopards Charles Okwemba sasa anasema ni wakati wa kuwa na mabadiliko ya kizazi katika timu ya taifa ya kandanda Harambee Stars. Okwemba amesema wachezaji wanaokuja katika timu za vijana wanahitaji kupandishwa katika timu ya wakubwa ili waweze kuonyeshwa zaidi na uzoefu unaohitajika kwa maendeleo. Stars ilishindwa kufuzu kwa Fainali za […]

MALUMBANO YA MCAS YATATIZA SHUGHULI KWENYE KAUNTI

Wawakilishi wadi katika baadhi ya mabunge ya kaunti nchini wameendelea kutatiza utoaji huduma kwa wakazi katika kaunti hizo kutokana na hali ya kutoelewana miongoni mwao, kaunti ya hivi punde ikiwa ni ya Kirinyaga ambapo wawakilishi wadi wamezozana kuhusu uongozi wa bunge hilo na kusambaratisha shughuli za kawaida. Hii ni baada yao kumtimua kiongozi wa walio […]

MAHANGAIKO ZAIDI VYUONI KUFUATIA MGOMO

Shughuli za masomo zimeendelea kutatizika katika vyuo vikuu vya umma nchini kwa wiki ya 4 sasa kufuatia mgomo wa wahadhiri ambao hii leo wameandamana jijini Nairobi na kuelekeza malalamishi yao katika majengo ya bunge, wizara ya fedha na ile ya elimu. Wakiongozwa na katibu mkuu wa muungano wa UASU Daktari Constantine Wasonga na mwenyekiti Grace […]

WAPE MTIHANI KAMA WAKO SAWA, OGAMBA

Huku masomo ya vyuo vikuu yakiendelea kuathirika kutokana na mgomo wa wahadhiri, waziri wa elimu Julius Ogamba amewataka wasimamizi wa vyuo hivyo kuwapa wanafunzi mitihani ya mwisho wa muhula iwapo wana uhakika kwamba wanafunzi wamepokea mafunzo ya kutosha. Akizungumza mapema leo baada ya uzinduzi wa usambazaji wa karatasi za mtihani wa KCSE katika kaunti ya […]

MGOMO VYUONI: OMTATAH ASHINIKIZA MAZUNGUMZO

Wakati uo huo, wito unaendelea kutolewa kwa serikali kutafuta suluhu kwa mgomo wa wahadhiri na kuwaepushia wanafunzi wa vyuo vikuu vya masaibu yanayowakumba ikiwemo kukaa vyuoni kwa muda mrefu Zaidi ya kawaida kabla ya kuhitimisha masomo yao. Wa hivi ni seneta wa Busia Okiya Omtatah ambaye ameutaja mgomo wa wahadhiri unaoendelea kama ambao umefikia hatua […]