RUTO AZUNGUMZIA MAUAJI DHIDI YA WANAWAKE

Vita dhidi ya mauaji yanayowalenga wanawake nchini vimepigwa jeki baada ya Rais William Ruto kutangaza mgao wa shilingi milioni 100 kwa kampeni inayolenga kutoa hamasisho dhidi ya mauaji hayo. Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi, Ruto amesema kuwa kampeni hiyo itaanza Jumatatu wiki ijayo ikilenga kutoa hamasisho kuhusu dhuluma za kijinsia. Aidha, amewataka wakenya kushirikiana dhidi […]

WAKAZI WA TRANSNZOIA WAHIMIZWA KUKUMBATIA MPANGO WA USALAMA

Wakazi wa eneo la Namanjalala moi farm kata ya Waitaluk kaunti ya Transnzolia wamehimizwa kuendelea kukumbatia mpango wa usalama ambao kulingana na wakazi utasaidia kudumisha amani na kukabiliana na utovu wa usalama katika eneo hilo. Katika kikao na wanahabari baada ya zoezi la kushirikisha umma kutekeleza wajibu wao kikatiba kuwachagua viongozi wao. Mwenyekiti wa mpango […]

WAKAZI WA BUSIA WATAKIWA KUJIANDIKISHA KWA SHA

Wito umetolewa kwa wakaazi wa kaunti ya Busia kuzidisha juhudi za kujiandikisha katika bima mpya ya afya kwa jamii SHA kwa manufaa yao binafsi. Gavana wa kaunti ya Busia Paul Otwoma amelalamikia idadi ndogo ya wakazi wa kaunti hiyo wanaojitokeza kujisajili kwenye SHA huku akitoa wito kwa viongozi wa kisiasa kujitolea kuwahamasisha wakazi wa Busia […]

ANDIENGO ALENGA KUBEBA TUZO KWA MAKALA YA AFRIKA

Mshindi wa medali ya fedha ya Ubingwa wa ndondi barani Afrika 2024 Elizabeth Andiego ameapa kupamba kabati yake ya kombe na sifa zaidi za kimataifa msimu huu. Andiego hana shauku ya kuendeleza mafanikio yake katika anga ya kimataifa baada ya kuonyesha maonyesho makubwa katika mashindano ya kwanza ya kila mwaka ya ndondi ya bara huko […]

KABRAS SUGAR WAKO KATIKA NAFASI BORA

Kocha mkuu wa mchezo wa raga katika shule ya upili ya Kakamega Amos Wamanga amedokeza kuwa Kabras Sugar RFC itaendeleza ubabe katika kombe la Kenya msimu mpya utakapoanza wikendi hii. Akizungumza na wanahabari Wamanga amesema ubora wa wachezaji na kina kikosi kinawafanya wapewe nafasi ya kutwaa taji hilo kwa mara ya nne mfululizo. Hata hivyo […]

NGALA APIGIA UPATO GOR KWA MASHEMEJI DERBY

Aliyekuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa Gor Mahia, Ronald Ngala ameiambia klabu hiyo kubadili msimamo na kuwashinda wapinzani wao AFC Leopards katika mechi ya Jumapili ya Mashemeji Derby licha ya ubovu wao. K’Ogalo imekuwa duni muhula huu wakishinda mechi mbili pekee kati ya sita na Ngala anaonya kuwa hii sio kiashirio cha kile cha kutarajia Jumapili. […]

NDOTO YA HARAMBEE STARS YASITISHWA

Kenya imejiondoa katika mchujo wa kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada ya kupata sare tasa dhidi ya vijana wenzao Namibia Jumanne alasiri katika Uwanja wa Peter Mokaba katika jimbo la Polokwane Limpopo nchini Afrika Kusini. Timu zote mbili ziliaga tumaini lao la kufuzu huku  pande zote mbili zilikuwa na nia ya […]

WATU SITA WAANGAMIA KWENYE MKASA WA MOTO

Maafisa wa usalama jijini Nairobi wameanzisha uchunguzi kufuatia mkasa wa moto ambao umesababisha vifo vya watu wasiopungua sita. Moto huo umezuka usiku wa kuamkia leo katika Kijiji cha Kitui kilichoko katika mtaa wa mabanda wa Majengo, eneo la Pumwani, jijini Nairobi. Kwa mujibu wa ripoti, watu wengine 19 wamejeruhiwa kwenye mkasa huo na wamekimbizwa hospitali […]

WAKAZI KIRINYAGA KUKOSA HUDUMA ZA BUNGE LAO

Wakazi katika kaunti ya Kirinyaga watalazimika kukosa huduma za bunge la kaunti hiyo baada ya vikao vya bunge hilo kuahirishwa kwa muda kufuatia mzozo wa uongozi ulioshuhudiwa hapo jana. Haya yanajiri baada ya makundi mawili bungeni humo kukosa kuafikiana kuhusu pendekezo la kumtimua kiongozi wa walio wengi Muriithi Kibinga ili kujaza nafasi yake na Geoffrey […]

WAKENYA WAENDELEA KUPINGA NYONGEZA YA USHURU

Wakenya kwa siku ya pili wamepata fursa ya kutoa maoni yao kuhusu miswada miwili ya wizara ya fedha inayopendekeza nyongeza ya ushuru, wakazi wa Mombasa wakionyesha kutoridhishwa na mapendekezo hayo. Kwa mujibu wa wakazi hao, nyongeza ya ushuru itaongeza mzigo wa Maisha ambayo tayari yamewalemea. Aidha, kamati ya bunge imekuwa na wakati mgumu kuwaeleza wakazi […]