SERIKALI YAKAZA KAMBA DHIDI YA KLINIKI NA SPA ZINAZOFANYA UPASUAJI HARAMU

Wamiliki wa kliniki za urembo na SPA ambazo ufanya upasuaji kinyume cha sheria wamejipata taabani baada ya wizara ya afya kuanzika msako mkali dhidi yazo Katibu wa Afya ya Umma, Mary Muthoni, amesema tathmini ilifanywa katika maeneo ya Nairobi, Mombasa, Nakuru, na Eldoret. Kati ya kliniki 26 zilizokaguliwa, 20 zilikuwa na leseni halali, tatu zilikuwa […]

IDARA YA UHAMIAJI YAWATAKA WAKENYA WACHUKUE VITAMBULISHO

Wakenya waliotuma maombi ya kupata vitambulisho vya kitaifa wameshauriwa kuzuru vituo vya uhamiaji nchini na kuchukua stakabadhi hizo, serikali ikisema takribani ya vitambulisho elfu 500 vingali katika vituo hivyo. Kwa mujibu wa katibu katika idara ya uhamiaji Julius Bitok, Zaidi ya kadi milioni 3 za Maisha zimekabidhiwa waliotuma maombi kufikia sasa, na kuwataka wakenya kujitokeza […]

MISHENI YA HAITI ITAENDELEA, MWAURA

Muda mfupi baada ya Marekani kutangaza kusimamisha shilingi bilioni 1.7 za kufadhili operesheni inayoongozwa na Kenya ya kurejesha utulivu nchini Haiti, serikali ya Kenya imesisitiza kwamba operesheni hiyo itaendelea. Kupitia taarifa, msemaji wa serikali Isaac Mwaura amesema kuwa misheni hiyo itafadhiliwa na fedha zilizokuwa zimeahidiwa kutolewa na hazina ya umoja wa mataifa, ambazo ni takribani […]

MGOMO: WAGONJWA MTRH WAHANGAIKA

Shughuli za matibabu katika hospitali ya rufaa na mafunzo ya Moi jijini Eldoret zimesambaratika kutokana na mgomo wa madaktari ambao umeanza hii leo, madaktari wakiapa kutorejea kazini hadi malalamishi yao yatakapoangaziwa. Miongoni mwa malalamishi ya madaktari hao ni wenzao kukaa kwa mkataba kwa muda mrefu bila kupewa ajira ya kudumu. Haya yanajiri huku wagonjwa wakihangaika […]

HARAMBEE STARS KUPATA KOCHA HIVI KARIBUNI

Kocha mkuu mpya wa Harambee Stars huenda atateuliwa hivi karibuni kufuatia mkutano kati ya Rais wa FKF Hussein Mohammed na maafisa wakuu wa Wizara ya Michezo. Waziri wa michezo Salim Mvurya na Katibu Mkuu katika wizara ya Michezo, Peter Tum wamesisitiza haja ya kuwa na kocha mwenye ujuzi wa kujenga timu ya ushindani kwa ajili […]

MILLAN WAMSAJILI JOAO FELIX

AC Milan imemsajili fowadi wa timu ya taifa ya Ureno Joao Felix kutoka Chelsea kwa mkopo kwa msimu uliosalia, wakati Chelsea wamemleta kiungo Mfaransa Mathis Amougou kutoka Saint-Etienne kwa kandarasi ya miaka minane. Ripoti za vyombo vya habari vya Uingereza zilisema Amougou, 19, alijiunga na Chelsea kwa ada ya takriban pauni milioni 12 ($14.98 milioni). […]

CITY THUNDER WAJIANDAA KWA MCHUANO MKALI

Licha ya kushindwa na mabingwa watetezi Nairobi City Thunder wikendi iliyopita, kocha mkuu wa Strathmore Blades Tony Ochieng amewapongeza wachezaji wake kwa uchezaji wao wa kuigwa. Ochieng anaamini vijana wake walijituma zaidi licha ya kupoteza 48-88 kwa mabingwa wa kitaifa katika mechi ya ligi kuu ya wanaume ya Mpira wa Kikapu nchini. Imetayarishwa na Nelson […]

EACC YAMKAMATA ALIYEKUWA DCIO WA LIKONI KWA TUHUMA ZA UFISADI

Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) imemkamata aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa makosa ya Jinai wa Wilaya ya Likoni (DCIO), Charles Onyango KA’galo. Msemaji wa EACC, Eric Ngumbi, amesema kuwa KA’galo amekamatwa katika nyumba yake ya kijijini huko Oyugis. Na kwamba anazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Port akisubiri kufikishwa mahakamani. Ngumbi amesisitiza […]

WASHUKIWA 2 WAKAMATWA KITENGELA KWA ULANGUZI WA BINADAMU

Polisi wame wameanzisha uchunguzi baada ya Washukiwa wawili wa ulanguzi wa binadamu kukamatwa baada ya kupatikana wakiwa na watu wengine 58 wenye asili ya ethiopia ndani ya nyumba moja huko Kitengela, Kaunti ya Kajiado. Ripoti ya polisi inaonyesha kuwa Daniel Nduati Kingoo, mwenye umri wa miaka 33, na Peter Maina Kimemia walikamatwa ndani ya nyumba […]

MAREKANI YASITISHA UFADHILI WA USALAMA WA UN KWA HAITI

Marekani imesitisha mchango wake wa dola milioni 13.3 kwa mfuko wa umoja wa mataifa UN unaofadhili kikosi cha usaidizi wa usalama nchini Haiti, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Rais Donald Trump kupunguza msaada wa nje. Baraza la Usalama la UN liliidhinisha kikosi hicho mnamo Oktoba 2023 kusaidia Haiti kupambana na magenge ya uhalifu. Hata […]