NAIROBI UNITED YAPANDISHWA DARAJA

Nairobi United inaadhimisha muongo mmoja tangu kuanzishwa kwake kwa mtindo wa kuvutia, ikiwa tayari imepanda daraja hadi Ligi Kuu ya FKF kwa kushinda taji la National Super League (NSL). Sasa, timu hiyo inalenga kutawaza msimu wake kwa kunyanyua Kombe la Mozzart Bet FKF katika fainali ya Jumapili dhidi ya mabingwa wa rekodi ya Ligi Kuu […]

FAITH ASHIKILIA IMANI

Bingwa wa olimpiki mara tatu Faith Kipyegon alibakisha sekunde 06.42 pekee aandikishe historia jana usiku , wakati nguli huyo alipomaliza muda mfupi tu wa kuwa mwanamke wa kwanza kukimbia maili moja katika chini ya dakika nne. Kipyegon alikimbia mbio hizo kwenye Uwanja wa Stade Charléty mjini Paris kwa dakika nne na 06. 42 sekunde, na […]

25 WAKAMATWA, BUNDUKI 5 ZAIBWA

Polisi wametangaza kuwa wamewakamata watu 25 wanaohusishwa na uharibifu wa mali ya serikali ikiwemo afisi na mahakama ya Kikuyu kaunti ya Kiambu wakati wa maandamano yaliyoshuhudiwa siku ya Jumatano. Kulingana na polisi, maandamano ya amani yaligeuka kuwa vurugu baada ya makundi ya wahuni waliokodishwa kutoka Limuru na Kiambu kuziba barabara ya Southern Bypass na Old […]

HAYAKUWA MAANDAMANO BALI MAPINDUZI- MURKOMEN

Maandamano yaliyofanywa Jumatano wiki hii yalilenga kuipindua serikali na wala hayakuwa ya kushinikiza haki kwa waathiriwa wa maandamano sawa na hayo ya mwaka jana. Ni kauli ya waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, akishutumu maandamano hayo na kuwaamuru polisi kuwapiga risasi watakaoonekana kutishia Maisha yao vituo vya polisi. Akiwahutubia wanahabari, Murkomen amedai kuwa waliopanga […]

WALIOPORA MALI NA KUHARIBU WATAANDAMWA, ASEMA MURKOMEN

Waziri wa usalama Kipchumba Murkomen ameonya kuwa waliohusika katika kupanga na waliopora mali wakati wa maandamano ya hapo jana watabeba msalaba wao. Ameahidi kuhakikisha kuwa walioathirika wakiwemo wanasiasa na maafisa wa serikali na wafanyibiashara wanapata haki. Murkomen anasisitiza kuwa maandamano ya hapo jana yalikuwa yamepangwa na lengo la kutekeleza uharibifu na kuwa waliofanya hivyo lazima […]

AROKO KUWA SHAHIDI KATIKA KESI YA MAUAJI YA WERE

Mfanyibiashara Philip Aroko aliyekamatwa baada ya kuhusishwa na mauaji ya mbunge wa Kaspul Ong’ondo Were sasa yuko huru na atakuwa shahidi katika kesi hiyo. Aroko aliyekana mashtaka dhidi yake ameachiliwa baada ya maafisa wa Dci kukagua Ushahidi uliokuwa umewasilishwa dhidi yake. Washukiwa wengine 3 wanaendelea kuzuiliwa akiwemo William Imoli,Edwin Oduor na Ebel Ochieng na wao […]

BABU OWINO ADAI KUPOKONYWA WALINZI

Mbunge wa Embakasi East Babu owino amedai kupokonywa walinzi baada ya kushiriki katika maandamano ya hapo jana, akitaja hatua hiyo kama shambulizi la moja kwa moja kwa uhuru wa kidemokrasia na jaribio la kuwatishia viongozi wanaodhubutu kusimama na wakenya. Kupitia mitandao ya kijamii, Owino ameshutumu uamuzi huo, huu ukiwa ni mwaka wa pili mfululizo kwake […]

WAFANYABIASHARA WAKADIRIA HASARA YA MAANDAMANO

Baada ya kupata nafuu kutokana na maandamano ya wiki jana ya Gen Z, wafanyabiashara wengi sasa wanahesabu hasara kufuatia maandamano ya hapo jana ambayo yalifanyika katika zaidi ya kaunti 25. Wafanyabiashara ambao wamezungumza na vyombo vya habari wamesema kuwa baadhi ya maduka yao yaliharibiwa na mali kuibiwa baada ya maandamano hayo, ambayo kwa kiasi kikubwa […]

MAGARI 26, PIKIPIKI 18 ZACHOMWA NYANDARUA- SERIKALI

Uharibifu zaidi wa mali ya serikali na ya kibinafsi imeendelea kuripotiwa nchini, siku moja baada ya maandamano ya kuwakumbuka waathiriwa wa maandamano ya mwaka jana. Katika kaunti ya Nyandarua, serikali ya kaunti hiyo imeripoti kuchomwa moto kwa magari yake 26 yaliyokuwa yameegeshwa katika afisi za kaunti ndogo ya Olkalou. Aidha, imesema pikipiki zake 18 zilichomwa, […]

!6 WAFARIKI KUTOKANA NA MAANDAMANO- AMNESTY

Ripoti zimeonyesha ongezeko la idadi ya watu walioafariki kutokana na maandamano ya hapo jana, ripoti za hivi punde zikiweka idadi hiyo kuwa watu 16, wengi wao wakiuawa na maafisa wa polisi. Mkurugenzi wa shirika la Amnesty Internationla Irungu Houghton, ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba idadi hiyo imethibitishwa na mashirika kadhaa, akisema waathiriwa 5 […]