KOCHA WA AFC LEOPARDS, FRED AMBANI, AMEMSIFU MSHAMBULIAJI VICTOR OMUNE

Kocha wa AFC Leopards, Fred Ambani, amemsifu mshambuliajiwa Harambee Stars, Victor Omune, kwa mchango wake muhimuuliowasaidia Ingwe kuibuka na ushindi wa 2–1 dhidi ya ShabanaFC katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Gusii.Ushindi huo umeendeleza rekodi ya kutopoteza mechi kwaLeopards kwenye Ligi Kuu ya SportPesa 2025, huku ukiongezapresha kwa Shabana ambao sasa hawajashinda katika mechi nnemfululizo.Shabana walitangulia […]

MARIGA ASEMA STARLETS WANA UWEZO WA KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2027

Makamu wa Rais wa Shirikisho la Soka Nchini (FKF), McDonaldMariga, anaamini kwamba timu ya taifa ya wanawake HarambeeStarlets ina uwezo wa kufuzu kwa Kombe la Dunia la Wanawakemwaka 2027 nchini Brazil, kufuatia uchezaji wao mzuri katikahatua za kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (WAFCON).Starlets walifuzu baada ya kuichapa Gambia kwa jumla yamabao 4–1 kwenye […]

DKT FRED MATIANG’I ATEULIWA KUWA MGOMBEA URAIS WA CHAMA CHA JUBILEE

Aliyekuwa waziri wa zamani Fred Matiang’i , ameteuliwa na baraza kuu la chama cha jubilee kuwa mgombea wa urais katika uchaguzi wa mwaka wa 2027 kwa tikiti ya chama hicho. Uamauzi huo umetangazwa  baada ya mkutano wa viongozi wakuu wa chama hicho hapa Nairobi, na katibu mkuu wa chama hicho jeremiah kioni Aidha ametangaza kuwa Matiang’i pia ameteuliwa kuwa naibu […]

MAAFISA WA KLINIKI KAUNTI YA MARSABIT WANAENDELEA NA MGOMO WAO

Maafisa wa kiliniki kutola kaunti ya Marsabit wameendelea na mgomo ambao umeingia wiki ya nne sasa. Mgomo huo umeendelea huku mvutano ukiendelea kuhusu mkataba uliosainiwa na serikali ya kaunti ya Marsabit na muungano wa maafisa hao wa kliniki mwezi aprili mwaka huu. Maafisa hao wa kliniki wanaitaka serikali ya kaunti sasa kuwajibika ipasavyo na kutekeleza matakwa yao. Imetayarishwa na Jones […]

MAHAKAMA YAFUTILIA MBALI USAJILI WA MAKURUTU WA POLISI

Mahakama ya uajiri na leba imefutilia mbali zoezi la kuwasajili makurutu wa kujiunga na idara ya polisi lililokuwa limeratibiwa kufanywa hivi karibuni, kwa misingi kwamba zoezi hilo lilikiuka katiba. Kwenye uamuzi wake, jaji Hellen Wasilwa, ameamuru kwamba tume ya huduma za polisi NPSC haina mamlaka ya kuwaajiri polisi, na kwamba hilo ni jukumu la kikatiba […]

DROO YA CARABAO

Bingwa mtetezi wa kombe la Carabao Newcastle United watachuana na Fulham katika awamu ya robo fainali ya kombe hilo, huku Arsenal wakiratibiwa kumenyana katika debi ya London na Crystal Palace. Palace walifuzu robo fainali jana usiku baada ya kuwatandika wanyonge wao Liverpool mabao 3-0 ugani Anfield, na hivyo kuwacharaza mabingwa hao wa Uingereza mara zote […]

DE BRYUNE AFANYIWA UPASUAJI

Kiungo wa kati wa klabu ya Napoli Kevin de Bryune amefanyiwa upasuaji wa msuli katika eneo la Antwerp nchini Ubelgiji baada ya kupata jeraha la msuli yaani hamstring alipocheza mkwaju wa penalti katika ushindi wao dhidi ya Inter Milan mwishoni mwa wiki. Katika taarifa, Napoli imetangaza kwamba upasuaji huo wa hapo jana ulikamilika salama, na […]

CHUI WA AFC WAIKWARUZA SHABANA

Klabu ya AFC Leopards iliikwaruza Shabana FC katika mechi ya kusisimua ugani Gusii mjini Kisii kwa kichapo cha mabao 2-1 hapo jana na kuiweka katika nafasi ya 5 kwenye msimamo wa ligi. Wenyeji Shabana walitangaza ubabe wao mwanzoni mwa mechi na kuchukua uongozi kupitia kwa fowadi wao Austin Odongo ila Leopards wakadinda kufyata mkia na […]

VIONGOZI WAONYA DHIDI YA KUVURUGA ZIARA YA RUTO 

Baadhi ya viongozi wa kisiasa katika kaunti ya Kakamega wamehimiza ushirikiano wa viongozi wote katika kaunti hiyo wakati wa ziara ya Rais William Ruto, wakisema hatua hiyo itahakikisha wanafaidika pakubwa kutokana na ziara hiyo. Rais amerataibiwa kuzuru maeneo kadhaa ya kaunti hiyo kuzindua miradi ya maendeleo, huku madai yakiibuka kwamba kuna njama ya vijana kutumiwa […]

MAHAKAMA KUWAHESABU WAFANYAKAZI WAKE LEO

Idara ya mahakama imeratibu zoezi la kupata hesabu ya wafanyakazi wake hii katika juhudi za kuimarisha usimamizi na uadilifu katika deta zake. Kupitia taarifa, jaji Mkuu Martha Koome amesema zoezi hilo linalenga kufanikisha mipango kuhusu wafanyakazi, kuimarisha uwajibikaji na kuhakikisha matumizi mwafaka ya raslimali katika mahakama zote nchini. Ameeleza kwamba zoezi hilo linalenga kutambua na […]