MAAFISA 4 NYAMIRA KUSHTAKIWA NA UFISADI

Maafisa 4 wakuu katika serikali ya kaunti y Nyamira wanatarajiwa mahakamani hii leo kufunguliwa mashtaka ya ufisadi baada ya kukamatwa hapo jana na maafisa wa tume ya kukabili ufisadi EACC. Mkurugenzi wa idara ya nyumba Lameck Machuki, mwezake wa barabara Peris Muse, afisa mkuu wa fedha Assanet Maube na mwenzake wa barabara Josphat Oruru walikamatwa […]

FAMILIA ZA AJALI YA NDEGE DIANI KUSUBIRI

Familia za waathiriwa wa ndege iliyowaua watalii 10 ambao ni raia wa kigeni na rubani raia wa Kenya katika eneo la Diani mapema Jumanne zitasubiri kwa hadi siku 30 kabla ya kufahamu chanzo cha ajali hiyo. Kulingana na katibu katika idara ya safari za angani Teresia Mbaika, muda huo utahitajika ili kukamilisha uchunguzi katika ajali […]

RUTO AAHIDI MAKAZI WA IDPS WA 2007

Hatimaye wakimbizi wa ndani kwa ndani kutokana na machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 wanatarajia mwanga wa tumaini la kupata makazi baada ya Rais William Ruto kutangaza mpango wa kuwatafutia ardhi. Akizungumza kwenye kaunti ya Nakuru wakati wa ziara yake, Rais Ruto ametangaza kwamba shilingi milioni 18 zitatolewa kufanikisha mpango huo unaolenga […]

WAHADHIRI WASISITIZA MASOMO HAYAPO VYUONI

Wizara ya elimu na wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma kwa mara nyingine wamekosa mwafaka kuhusu mgomo wa wahadhiri hao, ambao wamepinga ripoti ya wizara ya elimu kwamba masomo yamerejelewa katika baadhi ya vyuo vikuu vya umma. Viongozi wa muungano wa UASU wamesisitiza kuwa masomo yamelemazwa katika vyuo vikuu vyote vya umma na kwamba mgomo […]

WIZARA YA ELIMU YAZUIA MGAO KWA SHULE 29

Shule 29 zitasubiri kwa muda usiojulikana kabla ya kupokea mgao wa serikali kutokana na uchunguzi unaoendelea ili kuondoa shule na wanafunzi hewa kwenye orodha ya wizara ya elimu. Akizungumza akiwa mbele ya kamati ya elimu katika bunge la kitaifa, Waziri wa elimu Julius Ogamba amesema wizara hiyo imezuia mgao wa fedha kwa shule hizo baada […]

ALDRINE KIBET ATAJWA KIKOSINI HARAMBEE STARS

Timu ya taifa ya soka Harambee Stars itacheza mechi mbili zakirafiki za kimataifa mjini Antalya, Uturuki, wakati wa dirisha laFIFA mwezi ujao, kati ya Novemba 10 hadi 18.Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Shirikisho la SokaNchini Stars Itavaana na Madagascar tarehe 14 Novemba, kablaya kukutana na Comoros.Kocha mkuu Benni McCarthy ametangaza kikosi cha mwishokwa […]

KOCHA WA HARAMBEE STARLETS ASHUKURU MASHABIKI

Kocha mkuu wa Harambee Starlets, Beldine Odemba,amewapongeza na kuwashukuru mashabiki wa timu hiyo baadaya kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake(WAFCON) 2026 litakalofanyika nchini Morocco.Akizungumza mara baada ya ushindi wa bao 1–0 dhidi yaGambia kwenye mechi ya marudiano ya hatua ya mwisho yakufuzu iliyochezwa katika uwanja wa Stade Lat Dior mjini Thies,Senegal, Odemba […]

KOSKEI ASHTUMU UTENDAKAZI WA BAADHI YA TUME NCHINI

Mkuu wa utumishi wa umma Felix Koskei amesema kwamba ufisadi kwenye sekta ya umma umechangia kudorora kwa  uchumi wa taifa. Akizungumza kwenye uzinduzi rasmi wa tume ya mishahara nchini SRC, koskei ameshutumu utendakazi wa baadhi ya tume nchini ambazo hazitumikii wakenya ipasavyo ilhali zinapokea mishahara mikubwa. Imetayarishwa na Jones Koikai

MAONYESHO YA KILIMO YANG’OA NANGA JIJINI NAIROBI

Maonyesho ya Kimataifa ya Kilimo barani Afrika ya mwaka 2025 yamefunguliwa rasmi jijini Nairobi, chini ya kauli mbiu “Kuongeza Uzalishaji wa Kilimo barani Afrika kupitia Uvumbuzi na Upatikanaji wa Soko” kwa lengo la kuboresha ushirikiano wa China na Afrika katika kilimo cha kisasa. Katibu wa Kilimo nchini Paul Kipronoh Ronoh amesema maonyesho hayo yanalenga kuiweka Afrika kama kituo […]

RAUNDI YA 4 YA CARABAO KUMALIZIKA LEO

Kipute cha Carabao kinaendelea hii leo katika raundi ya 4 huku jumla ya mechi 9 zikisakatwa. Mabingwa watetezi Newcastle United watakuwa wenyeji wa Tottenham, Arsenal vs Brighton, Man City wakiwatembelea Swansea City nao Wolves wamalize udhia dhidi ya Chelsea ugani Molineux. Crystal Palace watakuwa wageni wa Liverpool, wakiwa tayari wamepambana mara 2 msimu huu, Palace wakiibuka na ushindi katika Community Shield na katika ligi kuu, na watalenga kuwalaza mabingwa […]