DROO YA CAF CONFEDERATIONS

Jumla ya klabu 16 zinasubiri kwa hamu kufahamu wapinzani wao katika awamu ya makundi ya mechi za mashirikisho bara Afrika yaani CAF Confederations Cup itakayoandaliwa tarehe 3 mwezi ujao nchini Afrika Kusini. Timu hizo, ikiwemo mwakilishi wa pekee wa Kenya Nairobi United, zilifuzu awamu ya makundi baada ya mkondo wa pili kutamatika wikendi iliyopita, zikijumuisha […]

NYOTA YA STARLETS KWENYE MIZANI

Timu ya taifa ya wanawake ya soka Harambee Starlets imekamilisha mazoezi yake kwa matayarisho yay a mechi ya leo ya mkondo wa pili ya kufuzu mashindano ya WAFCON mwaka ujao nchini Morocco. Starlets watakabiliana na The Gambia nchini Senegal kwenye mechi hiyo ya marudiano, wakiwa tayari wanaongoza kwa mabao 3:1 kufuatia ushindi wao wa mkondo wa kwanza, na sasa watahitaji […]

META, TIKTOK KUTII SHERIA ZA MIAKA 16 AUSTRALIA

Kampuni teknolojia za utoaji huduma za mitandao ya kijamii Meta na TikTok imetangaza kutii agizo la kuwazuia watoto walio chini ya umri wa miaka 16 nchini Australia kutumia mitandao hiyo, ingawa zikaonya kuwa huenda utekelezaji wa sheria hizo ukawa na changamoto. Sheria hizo zitaanza kutekelezwa tarehe 10 mwezi Disemba, ambako watumiaji walio chini ya miaka […]

VIJANA WEBUYE WAHIMIZWA KUCHUKUA KURA

Wakazi wa eneo bunge la Webuye West wametakiwa kujitokeza kwa wingi kusajiliwa katika zoezi linaloendelea la upigaji kura, idadi ndogo ikiripotiwa kufikia sasa. Kwa mujibu wa afisa wa tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC eneo hilo Bernard Mutali, huenda hali hiyo imechangiwa na umbali wa kituo ambako usajili huo unafanyika. Wakati uo huo, makundi ya vijana eneo […]

TUKO SERIKALINI, ODM

Chama cha ODM kitaendeleza ushirikiano wake na serikali ya Kenya Kwanza hadi mwaka 2027 na kwamba hakuna mgawanyiko chamani kuhusu ushirikiano huo. Haya yamebainika kwenye mkutano wa kwanza wa kamati kuu ya chama hicho tangu kifo cha aliyekuwa kinara wake Raila Odinga. Kwenye taarifa iliyosomwa na katibu mkuu Edwin Sifuna, ODM imetangaza kufanya mkutano maalum […]

CHANGAMOTO ZA KPSEA, KJSEA 

Mitihani ya kitaifa ya gredi ya 6 KPSEA na gredi ya 9 KJSEA inaingia siku ya pili hii leo huku changamoto kadhaa zikiripotiwa katika siku ya kwanza ya mitihani hiyo hapo jana. Miongoni mwa changamoto hizo ni baadhi ya shule kukosa kuwasajili watahiniwa, huku wanafunzi katika shule ya Endikir kaunti ya Kajiado wakianza mtihani wao […]

WANAHARAKATI WATAKA KUACHIWA KWA WENZAO

Mashirika ya kutetea haki nchini yameendelea kuzishinikiza serikali za Uganda na Kenya kuharakisha na kuwarejesha nchini wanaharakati Bob Njagi na Nicholas Oyoo walioripotiwa kutekwa nyara nchini Uganda zaidi ya mwezi mmoja uliopita. Miongoni mwa mashirika hayo ni chama cha wanasheria LSK, Amnesty International na Haki Africa, yakisema hali ya afya ya wawili hao imezorota. Imetayarishwa […]

MARUFUKU YA UKATAJI MITI YAONDOLEWA

Ni afueni kwa wafanyabiashara katika sekta ya mbao baada ya rais William Ruto kuondoa marufuku ya ukataji miti katika misitu ya umma nchini, hatua anayosema itabuni nafasi za ajira mbali ya kusitisha uagizaji wa fenicha. Rais aliondoa marufuku hiyo alipokuwa katika eneo la Elburgon kaunti ya Nakuru, na kutamatisha marufuku ya miaka 6 iliyowekwa ili […]

RUKU ATOA WITO WA KUFAFANULIWA UPYA KWA UTUMISHI WA UMA

Waziri wa  utumishi wa umma, Geoffrey Ruku , ametoa wito kwa serikali za Afrika kufafanua upya jukumu la utumishi wa umma kama swala kuu katika  mageuzi ya kiuchumi barani Afrika. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa programu ya utawala bora wa kiuchumi  jijini Nairobi, Ruku amesema ustawi wa Afrika unategemea utawala bora, uvumbuzi na uongozi wa kimaadili. Imetayarishwa na Jones Koikai

RAIS RUTO AMEANZA ZIARA YAKE YA SIKU TATU KAUNTI YA NAKURU

Rais William Ruto ameanza ziara ya siku tatu katika kaunti ya Nakuru, akiwa na lengo  la kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo ujenzi wa barabara ya Kinamba kuelekea Mengich, Murionduko na Kuresoi kaskazini . Miradi hiyo inaolenga kuboresha miundombinu na kuimarisha uchumi wa eneo hilo. Aidha, ameongoza shughuli ya upanzi wa miche elfu tano katika msitu wa mau, kama […]