ROBO TATU YA KAMPUNI NCHINI ZASHINDWA KULIPA KODI

Ni pigo kwa mamlaka ya ushuru KRA baada ya takwimu za mwaka wa kifedha unaoisha Juni 2025, kuonyesha kuwa kampuni 156,232 pekee  zililipa ushuru wa mapato ya shirika (CIT), ikiwa ni asilimia 25.2 ya kampuni zote zinazofanya kazi nchini. Kulingana na ripoti kutoka mamalaka hiyo, kampuni 461,969 kati ya kampuni 618,201 zilizosajiliwa zilishindwa kutimiza majukumu yao ya ushuru licha ya dhuluma […]

KENYA IKO MBIONI KUJIANDAA KWENYE MICHEZO YA OLIMPIKI YA GOFU

Mbio za kuelekea Michezo ya Olimpiki ya Los Angeles 2028 zinaendelea kwa wachezaji wa gofu wa Kenya huku PGK Equator Tour ikiingia kwa mkondo wake wa tano wiki hii katika Klabu ya Gofu ya Nakuru ya par-73 katika Kaunti ya Nakuru. Mechi hiyo inatazamiwa kuchezwa Alhamisi hadi Jumapili, Oktoba 5, huku zaidi ya wataalamu 40 […]

ASENALI YAKANYAGA OLYMPIAKOS

Arsenal walipata ushindi wa mabao mawili kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya huku bao la dakika za lala salama la Bukayo Saka likifikisha ushindi wa 2-0 dhidi ya Olympiakos kwenye Uwanja wa Emirates. Saka, aliyetokea kama mchezaji wa akiba kipindi cha pili, alipiga shuti na kupita kipa wa Olympiakos, Kostas Tzolakis kutoka pasi ya Martin Odegaard […]

NAIVAS FC INASAKA KUENDELEZA USHINDI KATIKA LIGI YA NSL

Timu ya Naivas FC itasaka kuendeleza kasi yake ya mapema katika ligi ya daraja la pili Jumamosi hii dhidi ya MCF. Wachezaji hao walianza kampeni yao kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Fortune Sacco katika mechi yao ya ufunguzi wa msimu wikendi iliyopita, matokeo ambayo yaliwaweka nafasi ya tano kwenye jedwali, sawa na viongozi wa […]

BUNYORE STARLETS WAKO TAYARI KWA MSIMU HUU MPYA

Bunyore Starlets wanajiandaa katika Ligi Kuu ya Taifa ya Wanawake (NSL) wakiwa na matumaini mapya, baada ya kuimarisha kikosi chao na benchi ya ufundi. Mwenyekiti wa klabu Moses Mabwa ameonyesha imani kwamba nyongeza hizo mpya zitasaidia kuendeleza ajenda ya klabu. Starlets watakuwa wenyeji wa Kitale’s Royal Starlets katika mechi yao ya ufunguzi ya NSL itakayofanyika […]

MAKOMREDI KUANZA MGOMO LEO

Wanafunzi wa vyuo vikuu vya umma wameratibiwa kujiunga na wahadhiri wao kwenye mgomo wa kitaifa hii leo kwa lengo la kuishinikiza serikali kutatua mgomo wa wahadhiri ili kufanikisha kurejelea shughuli za masomo. Viongozi wa wanafunzi hao wamesema wanahofia huenda mgomo huo ukaathiri kalenda ya masomo yao iwapo hautatuliwa mapema, huku wahadhiri wakishikilia kuwa hawatarejea kazini […]

SHA YAMULIKWA KUHUSU UAJIRI WAKE

Washikadau mbali mbali wameendelea kushinikiza uchunguzi huru kufanywa katika Sakata ya ajira kwenye mamlaka ya afya ya jamii SHA baada ya ripoti kuibuka kwamba mhasibu Andrew Rotich aliyefichua ulaghai wa mamilioni ya pesa ameachwa nje ya orodha ya walioteuliwa upya. Wa hivi punde ni chama cha wahasibu ICPAK, ambacho kimetaka maelezo kuhusu mchakato wa ajira […]

IEBC YATAKIWA KUWAHAMASISHA WAPIGA KURA

Baadhi ya wakenya wameitaka tume ya IEBC kutoa hamasisho kwa wakenya kuhusu umuhimu wa kupiga kura ili kuhakikisha kuwa idadi kubwa inafahamu na kujitokeza kusajiliwa kama wapiga kura kwneye zoezi linaloendelea nchini. Hii ni baada ya idadi ndogo kujitokeza, vingi vya vituo vya usajili vikirekodi chini ya watu 10 kwa siku wanaojitokeza. Hata hivyo, IEBC […]

WABUNGE WA UPINZANI KUPINGA MSWADA MAHAKAMANI

Baadhi ya wabunge wa upinzani wametishia kuelekea mahakamani kupinga mswada wa kubinafsishwa kwa shirika la Kenya Pipeline iliyopitishwa hapo jana bungeni, wakisema haukuhusisha maoni ya wananchi. Katika kikao cha kujadili na kupitisha hoja hiyo, wabunge hao waliondoka bungeni wakipinga uamuzi wa kupitishwa kwa mswada huo. Hata hivyo, waliounga mswada huo wakiongozwa na kiongozi wa walio […]

EPRA YAFUNGA VITUO 10 VYA MAFUTA KUTOKANA NA UCHAKACHUAJI

Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli (EPRA) imefunga vituo 10 vya mafuta nchini kwa kuuza mafuta yaliyochakachuliwa au yanayopaswa kusafirishwa nje ya nchi kati ya Julai na Septemba 2025. Hatua hiyo ilifuatia majaribio 6,090 yaliyofanywa katika vituo 1,315, huku 1,303 zikipatikana zinafuata kanuni. Vituo vingine viwili vilifeli majaribio—kimoja kipo mahakamani, huku kingine kikiendelea na kazi baada ya kulipa faini […]