KYLLIAN MBAPPE YUKO SAWA, DESCHAMPS

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ufaransa Didier Deschamps amethibitisha kuwa mshambulizi matata wa timu hiyo na klabu ya Real Madrid Kylian Mbape yuko sawa kushiriki mechi ya kuwania kufuzu katika kombe ka dunia litakaloandaliwa mwaka ujao. Mbappe ambaye amekuwa tegemeo kwa Les Blues msimu huu, aliondoka uwanjani akichechemea mwishoni mwa mechi kati ya […]

STARS MBIONI KUREJESHA NYOTA

Timu ya taifa ya soka Harambee Stars imeonyesha imani ya kuibuka na ushindi katika mechi zake 2 zilizosalia kabla ya kuaga rasmi kinyang’anyiro cha kufuzu kombe la dunia mwaka ujao litakaloandaliwa katika mataifa ya Marekani, Mexico na Canada. Stars watamenyana na Burundi Alhamisi hii jijini Bunjumbura kabla ya mechi ya mwisho jijini Abidjan Ivory Coast […]

RAIS AJIUZULU KUTOKA WADHIFA ALIOPEWA

Azma ya serikali kuwafidia waathiriwa wa maandamano imepata pigo jingine baada ya Rais wa chama cha wanasheria LSK Faith Odhiambo kujiuzulu kutoka wadhifa wa makamu wa mwenyekiti wa jopokazi lililoteuliwa kuongoza juhudi hizo. Kwenye waraka wake, Odhiambo ametaja shughuli zilizokwama kutokana na amri ya mahakama huku akisisitiza haja ya marekebisho mapanma ya haki. Ameongeza kuwa […]

MAGAVANA, KMPDU ZAVUTANA KUHUSU IDADI YA VIFO

Baraza la magavana limepinga ripoti kuhusu ongezeko la vifo vya Watoto wanaozaliwa kufuatia mgomo wa madaktari katika kaunti ya Kiambu, wakitaja ripoti hizo kuwa zenye nia ya kuudhalilisha ugatuzi nchini. Mwenyekiti wa baraza hilo Ahmed Abdullahi akizungumza baada ya mkutano wa baraza hilo, ameushutumu muungano wa madaktari KMPDU kwa madai ya kuweka idadi hiyo juu […]

UGANDA YAKANA KUWATEKA WAKENYA

Kitendawili kimeibuka kuhusu waliko wanaharakati wawili wa Kenya Bob Njagi na Nicholas Oyoo walioripotiwa kutekwa nyara nchini Uganda baada ya idara ya polisi nchini Uganda kukana kuhusika na utekaji nyara wa wawili hao. Msemaji wa polisi wa Uganda Kituuma Rusoke, amesema hana taarifa kuhusu waliko wanaharakati hao, ambao kulingana na walioshuhudia, walitekwa nyara wiki jana […]

UPINZANI: KALONZO HAJI

Viongozi wa mrengo wa upinzani wamekariri kuwa kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka hayuko tayari kujiunga na serikali ya Kenya Kwanza, wakiitaka serikali kusitisha juhudi za kumrai ajiunge nayo. Wakiongozwa na aliyekuwa naibu rais Rigathi Gachagua, Martha Karua wa PLP na Eugene Wamalwa wa DAP-K baada ya kujiunga na Musyoka kwenye ziara ya Ukambani, viongozi hao […]

ALIYEKUWA CHIFU WA EASTLEIGH KASKAZINI AHUKUMIWA

Mahakama ya rufaa jijini nairobi imeidhinisha hukumu ya aliyekuwa chifu wa Eastleigh kaskazini ,Paul Kuria kwa madai ya kupokea hongo kutoka kwa mkaazi mmoja akitaka stakabadhi za uraia kwa jamaa zake. Katika utetezi wake, ngugi amedai kuwa alikamatwa na maafisa wa tume ya maadili na kupambana na ufisadi eacc, akisema kwamba kukamatwa kwake kulichochewa kisiasa.  Mahakama ya rufaa ilitupilia mbali […]

SERIKALI YAONDOA ADA ZA KUPATA UPYA VITAMBULISHO ILI KUONGEZA USAJILI WA WAPIGA KURA

Mwananchi sasa ana kila sababu ya kutabasamu baada ya Rais William Ruto kutangaza kuondoa kwa muda ada ya kupata upya vitambulisho vya kitaifa ili kuhakikisha Wakenya wote wanaostahiki wanajiandikisha kama wapiga kura. Akizungumza katika kaunti ya Vihiga Rais amesema ada hiyo iliyoanzishwa awali ilikuwa na lengo la kudhibiti matumizi mabaya ya huduma hiyo na itasitishwa […]

WABUNGE WAPENDEKEZA KUPUNGUZWA BEI YA UMEME MARA SITA

Huenda wakenya wakafurahia umeme wa bei nafuu ikiwa pendekezo la Kamati ya Nishati ya Bunge la Kitaifa la kupunguza bei ya jumla ya umeme kwa Ksh9.04 kwa kila kilowati kwa makubaliano mapya ya ununuzi wa umeme litapitishwa. Kwa sasa, baadhi ya kampuni huuza umeme kwa Kenya Power kwa hadi Ksh56 kwa kilowati kila saa, na hivyo kufanya kuwa […]

UBASHIRI WAONYA KUHUSU MAFURIKO

Idara ya utabiri wa hali ya anga imewataka wakenya kutahadhari kuhusu uwezekano wa mafuriko kutokana na mvua inayoendelea katika maeneo mbali mbali ya nchi. Kulingana na idara hiyo, huenda mvua inayoendelea ikaandamana na upepo mkali na ngurumo za radi, maeneo yaliyo katika nyanda za chini yakirataibiwa kuwa na mafuriko. Wakenya wameshauriwa kutopita katika maji ya […]