OGAMBA AWARAI WAHADHIRI KUELEWA HALI

Huku shughuli za masomo zikilemazwa katika vyuo vikuu vya umma kwa siku 50 kutokana na mgomo wa wahadhiri, Waziri wa elimu Julius Ogamba ametoa wito kwa wahadhiri kukubali malipo kwa awamu 2 na kurejea kazini ili kuokoa hali vyuoni. Kwa mujibu wa Ogamba, serikali kukubali kutoa malipo hayo japo kwa awamu hizo, ni ishara ya […]

UKATILI WA MAFURIKO TRANS NZOIA

Zaidi ya familia 3,000 katika maeneo ya Namanjalala na Kapomboi kaunti ya Trans Nzoia zinalilia msaada wa dharura kutokana na mafuriko baada ya mto Sabwani kuvunja kingo zake na kuwaacha bila makao. Mafuriko hayo yamesomba mashamba na makazi, waathiriwa wakikabiliwa na athari za magonjwa mbali na hasara kutokana na uharibu wa mazao yao. Waathiriwa wamehimiza […]

MBINU MBOVU ZA UKULIMA KIINI CHA VIFO ELGEYO MARAKWET, MURKOMEN

Ukataji miti kiholela na mbinu mbovu za ukulima ndicho chanzo cha maporomoko ya ardhi ambayo yamewaua watu 26 kufikia sasa mbali na uharibifu mkubwa katika eneo la Chesongoch kaunti ya Elgeyo Marakwet. Haya ni kulingana na Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen ambaye ametaja mkasa huo kuwa wa kitaifa, akiwataka waathiriwa kuhamia maeneo yaliyotajwa […]