MBUNGE KAKAI ASHINIKIZA SULUHU YA KUDUMU KWA MAFURIKO

Serikali imetakiwa kusaka makazi ya kudumu kwa waathiriwa wa mafuriko ambao huathirika kila msimu wa mvua katika kaunti ya Trans Nzoia, ili kuwaondolea mahangaiko ya kukosa makazi. Katika kikao na wanahabari baada ya kutoa misaada kwa waathiriwa katika eneo la Machungwa, mbunge wa Kiminini Kakai Bisau, amesema hiyo ndiyo njia mwafaka ya kuepusha hasara ya […]

IEBC YAPUZILIA MBALI KUJIONDOA KWA MWANIAJI MALAVA

Utata umeibuka kuhusu mwaniaji wa chama cha DCP Edgar Busiega kujiondoa kwenye uchaguzi mdogo unaokuja eneo bunge bunge la Malava, baada ya tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC kupuzilia mbali madai hayo. Akizungumzia utayarifu wa uchaguzi huo, afisa wa IEBC anayesimamia uchaguzi huo Salim Abdalla amezitaja taarifa hizo kuwa uvumi, na kwamba mwaniaji huyo […]

NCIC IMESHINDWA KUZUIA UCHOCHEZI, MASENETA

Tume ya kitaifa kuhusu utangamano na uwiano NCIC imetakiwa kukaza Kamba na kukabili cheche za uchochezi katika mitandao ya kijamii nan je ya mitandao hiyo ili kuepusha taifa kutumbukia katika ghasia za baada ya uchaguzi jinsi ilivyoshuhudiwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007. Ni wito uliotolewa na maseneta baada ya mkurugenzi mkuu wa NCIC […]

MERINO AIWEKA MERIKEBU YA ARSENAL KWENYE MKONDO

Mikel Merino alifunga mara 2 na kuwapa Arsenal ushindi dhidi ya Slavia Prague katika awamu ya 4 ya mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya, na kuongeza ushindi wa mechi 10 bila kikomo kwa The Gunners katika mashindano yote. Aidha, hii ilikuwa mechi ya 8 mfululizo ya Arsenal kutofungwa bao, wakifikia rekodi yao iliyowekwa katika misimu […]

Wabaya Bayern wamzima bingwa PSG

Pambano la kubaini timu bora barani Ulaya baina ya bingwa mtetezi wa klabu bingwa barani Ulaya PSG ya Ufaransa na miamba wa soka wa Ujerumani Bayern Munich liliishia kwa bingwa kudhalilishwa nyumbani na wachezaji 10 wa Bayern baada ya kugaragazwa mabao 2-1. Kiungo wa zamani wa Liverpool Luiz Diaz alijitwika jukumu la kuwafungia mabingwa hao […]

LIVERPOOL WAWAWEKA LOS BLANCOS GIZANI

Miamba wa soka nchini Uingereza Liverpool walirejelea ubora wao na kuwafundisha Los Blancos wa Real Madrid namna ya kucheza soka na kupata ushindi muhimu katika mtanange wa klabu bingwa barani Ulaya ugani Anfield jana usiku. Ushindi wa bao 1-0 ukijiri baada ya vijana hao wa Arne Slot kutamatisha msururu wa kupoteza mechi 6 kati ya […]

VIHIGA QUEENS WALENGA KUREJELEA UBINGWA KWPL

Meneja wa klabu ya Vihiga Queens inayosakata ligi kuu ya wanawake nchini KWPL Boniface Nyamunyamuh, anasema kikosi chake kinalenga kurejelea ubingwa wa taji hilo msimu huu na kwamba atafanya kila awezalo kuhakikisha ndoto hiyo inatimia. Nyamunyamuh aliyewaongoza vipusa hao kumaliza katika nafasi ya 3 msimu jana kwa alama 41, zikiwa alama 8 nyuma ya mabingwa […]

WANASIASA, WAFUASI WAONYWA KABUCHAI

Idara ya usalama katika eneo la Bungoma Central imetoa onyo kwa viongozi wa kisiasa na wafuasi wao dhidi ya kuzua vurugu kwenye kampeni zinazoendelea ya uchaguzi mdogo katika wadi ya Chwele-Kabuchai jinsi imekuwa ikishuhudiwa. Akizungumza baada mkutano wa kiusalama eneo hilo, kamishna wa kaunti ya Bungoma Thomas Senkei ametoa tahadhari hiyo, akisema watakaopatikana watachukuliwa hatua […]

WAHADHIRI WALEGEZA MSIMAMO, ILA…

Wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma wako tayari kusitisha mgomo wao wa siku 49 na kurejea kazini iwapo serikali itawalipa asilimia 80 ya pesa wanazodai kwenye mkataba wa maelewano wa mwaka 2017-21. Mbele ya kamati ya elimu katika bunge la kitaifa, viongozi wa miungano ya UASU na KUSU wamepinga pendekezo la serikali kuwalipa fedha hizo […]

CHUO KIKUU CHA EGERTON CHAFUNGWA KWA MUDA

Wanafunzi katika chuo kikuu cha Egerton wana hadi saa nane mchana hii leo kuondoka chuoni humo kufuatia uamuzi wa baraza kuu la chama hicho kusitisha kwa muda shughuli za masomo kutokana na mgomo wa wahadhiri na wafanyakazi wa vyuo vikuu. Kupitia notisi, chuo hicho kimesema mgomo unaoendelea umeathiri pakubwa shughuli chuoni humo, na hivyo pana […]