KENYA YAVUNJA REKODI BARANI AFRIKA MPIRA WA VIKAPU

Kenya imevunja rekodi ya kuwa timu ya kwanza barani Afrika kufuzu katika kategoria mbili za wanawake na wanaume katika mashindano ya Commonwealth ya mchezo wa vikapu wa 3×3 yatakayoandaliwa jijini Glasgow, Scotland baadaye mwaka huu. Timu ya wanawake iliweka msingi wake wa kufuzu mnamo mwaka 2023, walipoichabanga Misri 21-20 katika kombe la FIBA Africa 3×3, […]

LIONESSES WAREJEA NCHINI

Kikosi cha timu ya taifa ya raga, Kenya Lionesses, kimerejea nchini katika uwanja wake wa mazoezi wa RFUEA kutoka nchini Uhispania, walikokuwa wakifanya mazoezi ya wiki moja kwenye maandalizi ya dimba la HSBC 7s Division 2 litakaloandaliwa tarehe 14 na 15 mwezi huu katika uwanja wa Nyayo. Mkufunzi mkuu wa timu hiyo Simon Odongo, amesema […]

KAGAME AITAKA RWANDA ‘KUJITEGEMEA’

Rais wa Rwanda Paul Kagame, amewahimiza wananchi wake kuimarisha mikakati ya kujitegemea huku wito wa kutaka Amerika iiwekee vikwazo nchini hiyo ukiongezeka. Rwanda imekuwa ikikosolewa na jamii ya kimataifa kuhusiana uungwaji wake mkono wa kundi la wapiganaji la M23 Mashariki wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, ingawa Rwanda imekuwa ikisema kuhusika kwake nchini humo […]

RUTO ATETEA MIRADI YAKE

Rais William Ruto ameendelea kutetea miradi inayotekelezwa na serikali yake licha ya ukosoaji kutoka kwa viongozi wa upinzani, akisema miradi hiyo inalenga kuboresha maisha ya wakenya. Akizungumza mjini Malindi alikoongoza hafla ya kuwapa vijana fedha chini ya mradi wa NYOTA, Rais Ruto amesema mradi huo ni suluhisho kwa tatizo la ukosefu wa ajira nchini, akiwataja […]

ODM YAPINGA MAGEUZI YA UONGOZI AZIMIO

Mageuzi ya hivi punde ya uongozi katika muungano wa Azimio yameendelea kuibua mvutano kwenye muungano huo, chama cha ODM sasa kikiyapuzilia mbali kwa misingi kwamba kinara wake Oburu Oginga hakushirikishwa wala kuhusishwa. Kulingana na ODM, mabadiliko hayo yaliyotangazwa na Rais Mstaafu Uhuru Kenyatta, ni batili na kinyume na sheria za muungano huo, ikimtaka msajili wa […]

WAATHIRIWA WA GHASIA 2007 WAJUMUISHWE- WADAU

Baadhi ya wakenya wameitaka serikali kuwajumuisha waathiriwa wa machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2008 kwenye mpango wa kuwapa fidia waathiriwa wa maandamano, wakisisitiza kuwa baadhi ya waathiriwa hao wanaishi katika hali ngumu. Wakizungumza jijini Kisumu wakati wa vikao vya kukusanya maoni ya wakenya kuhusu mpango huo vinavyoendeshwa na kamati iliyoteuliwa kuangazia utekelezaji […]

SERIKALI YATAKIWA KUCHUNGUZA AJIRA URUSI

Serikali imetakiwa kuchukua hatua za dharura na kuchunguza zoezi la usajili wa wakenya wanaolenga kuelekea nchini Urusi kwa ajira, kutokana na vifo vya wakenya kadhaa nchini humo baada yao kushurutishwa kujiunga na jeshi la taifa hilo. Kwenye hafla ya mazishi ya mmoja wa waliofariki nchini humo, Charles Waithaka katika kaunti ya Nyeri iliyofanyika bila mwili […]

MAKALI AOMBA SUBIRA KWA WAFANYAKAZI WA SUKARI

Mbunge wa Kanduyi John Makali amewaomba wafanyakazi wa viwanda vya sukari katika mkoa wa Magharibi kuwa na subira huku serikali ikiendelea kushughulikia ulipaji wa malimbikizi ya mishahara yao. Akizungumza katika kaunti ya Bungoma, Makali ametoa hakikisho kuwa serikali iko mbioni kuhakikisha wafanyakazi pamoja na wakulima wa miwa wanalipwa fedha wanazodai kwa wakati unaofaa. Hata hivyo, […]

WAZOA TAKA DANDORA WASHINDA KESI

Mahakama ya Mazingira na Ardhi ya Milimani imeamuru kulipwa fidia ya shilingi milioni 25.8 kwa wazoa taka 1,032 wanaofanya kazi katika dampo la Dandora, baada ya kubaini kuwa haki zao za kikatiba zilikiukwa kutokana na kuathiriwa kwa muda mrefu na uchafuzi wa hewa. Katika uamuzi wake, Jaji Anne Omollo ameamua kwa niaba ya wazoa taka hao dhidi ya Serikali […]

SERIKALI KUIMARISHA UTAFITI NA UBUNIFU VYUONI

Rais William Ruto amesema Serikali inaweka utafiti na ubunifu kuwa nguzo kuu katika mafunzo ya elimu ya juu ili kukuza maarifa na ushindani wa taifa. Ruto amesema kuanzishwa kwa idara maalum ya serikali ya sayansi, utafiti na ubunifu kunadhihirisha dhamira ya kitaifa ya kuimarisha mafunzo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati, (STEM). Aidha Ruto Amesisitiza kuwa hatua hiyo […]