BIDCO YAANZA KUONYESHA DALILI ZA KUIMARIKA

Kocha mkuu wa Bidco United Anthony “Vieira” Akhulia amechukua jukumu kamili kwa msimu mgumu wa klabu hiyo akisisitiza kuwa timu inaonyesha dalili za kuimarika licha ya kuwa kwenye hatari ya kushuka daraja. Akizungumza baada ya sare ya bao 1–1 ugenini dhidi ya Kenya Police FC, Akhulia amesema msimu ulianza kwa matumaini makubwa kabla ya mambo […]

MAHAKAMA YAONGEZA AMRI YA KUZUIA MALI ZA WAMATANGI

Mahakama Kuu imeongeza muda wa amri za muda za kuzuia matumizi au uhamishaji wa mali katika kesi ya madai ya ufisadi inayomkabili Gavana wa Kiambu Paul Kimani Wamatangi na wengine. Kesi hiyo, inayosikilizwa na Jaji Hedwig Okwany katika Kitengo cha Makosa ya Kiuchumi na Ufisadi, inahusisha juhudi za Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi […]

AJALI YA BODA BODA YAUA MWANAMKE BUSIA

Mwanamke mwenye umri wa makamo ameaga dunia kufuatia ajali ya barabarani iliyohusisha boda boda katika eneo la Mlango Kumi, kwenye barabara kuu ya Busia kuelekea Kisumu. Ajali hiyo ilitokea mapema hii leo, huku chanzo chake kikisalia kutambuliwa na maafisa wa polisi waliowasili eneo la tukio kufanya uchunguzi. Abiria wengine wawili waliojeruhiwa katika ajali hiyo walikimbizwa katika […]

RUTO ANA NAFASI YA MUHULA WA PILI 2027

Mbunge wa Gem Elisha Odhiambo amesema ana imani kuwa Rais William Ruto atachaguliwa tena kwa muhula wa pili katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2027. Akizungumza katika kaunti ndogo ya Gem Wagai, kaunti ya Siaya, Odhiambo amesema mafanikio ya serikali ya Kenya Kwanza katika kuleta maendeleo katika maeneo mbalimbali ya nchi ndiyo msingi wa imani hiyo. […]

MARAGA: SERIKALI YAENDESHWA KWA UONGOZI MBAYA

Aliyekuwa Jaji Mkuu na mwaniaji wa urais kupitia chama cha United Green Movement (UGM), David Maraga, amesema serikali inaendesha taifa kwa njia isiyofaa kutokana na uongozi mbaya. Akizungumza Kaunti ya Kwale, wakati wa kuhamasisha wananchi kujiandikisha kama wapiga kura, Maraga amesema ufisadi umekithiri katika idara muhimu za serikali na kuwalaumu watumishi wa umma kwa kupora […]

IEBC YAZINDUA MPANGO WA USAJILI WA WAPIGA KURA KIDIJITALI

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) imetangaza mpango wa kuzindua jukwaa la kidijitali litakalorahisisha zoezi la usajili wa wapiga kura, hasa kwa vijana. Mwenyekiti wa IEBC Erastus Ethekon amesema jukwaa hilo litaruhusu wanaojiandikisha kujaza taarifa zao mtandaoni kabla ya kufika vituo vya usajili kuweka alama za kibayometriki. Ethekon ame ongeza kuwa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu […]

RUTO AKUTANA NA WAGOMBEA WA UDA IKULU

Rais William Ruto anaongoza mkutano na wagombeaji 12,353 wa nyadhifa mbali mbali kwenye uchaguzi mkuu ujao kupitia tiketi ya chama cha UDA kupanga mikakati ya chama hicho kuelekea kwenye uchaguzi huo. Mkutano huo unafanyika katika Ikulu ya Nairobi, ukiwaleta Pamoja wagombeaji hao wakiwemo walio madarakani, ambako Rais Ruto amekariri ajenda ya Bottom Up. Imetayarishwa na […]

KINDIKI: NYOTA KUWAFIKIA MILIONI 2

Mradi wa ujasiriamali wa serikali wa NYOTA unalenga kupanuliwa ili kuwafaidi vijana zaidi ya milioni 2 kote nchini, tayari vijana 820,000 wakiwa wamelengwa Haya ni kulingana na naibu Rais Kithure Kindiki, akisema lengo la mradi huo ni kuona vijana wengi wamepata mafunzo na mtaji wa kuendesha biashara ili kujikimu kiuchumi. Jumla ya vijana 121,000 wamepokea […]

KANUNI MPYA ZA KRA ZA KUKUSANYA USHURU MWAKA HUU

Mamlaka ya kukusanya Ushuru nchini (KRA) imebadilisha jinsi inavyokagua ripoti za ushuru wa mapato, na hivyo kuashiria mabadiliko makubwa katika utekelezaji wa ushuru. Tangia mwezi Januari mwaka huu, mamlaka hiyo itathibitisha kila takwimu iliyotangazwa katika marejesho ya kodi ya mapato dhidi ya data ya kielektroniki ya wakati halisi wakati wa kuwasilisha. Chini ya mfumo mpya, […]

ARSENAL WATINGA FAINALI TANGU 2018

Klabu ya Arsenal ya Uingereza imekariubia kushinda taji kuu la kwanza tangu mwaka 2020, baada ya kuitandika Chelsea jumla ya mabao 4-0 na kutinga fainali ya taji la Carabao Cup. Wakiwa wanaongoza 3-2 kutoka kwenye mkondo wa kwanza wa nusu fainali, the Gunners walisubiri hadi dakika ya 97 kabla ya kujihakikishia tiketi ya kuingia ugani […]