MALKIA STRIKERS WASEMA WAKO TAYARI

Nahodha wa Malkia Strikers, Trizah Atuka amesema timu iko tayari kwa majukumu ya Kombe la FIVB Challenger na Michezo ya Olimpiki. Atuka mwenye umri wa miaka 32 ana uhakika mabingwa hao mara kumi wa Afrika watatangaza uwezo wao katika majukumu hayo mawili licha ya kuonekana kuwa wanyonge. Atuka amewapongeza wadhamini ambao wamejitokeza ili kuongeza maandalizi […]

RUTO ATII SHINIKIZO ZA MSWADA

Hatimaye Rais William Ruto amekataa kutia Saini na kuutupilia mbali mswada wa fedha wa mwaka 2024 baaad ya shinikizo kutoka kwa Wakenya. Katika hotuba kwa taifa kutoka Ikulu ya Nairobi, Ruto amesema amechukua hatua hiyo kama njia ya kukubaliana na uamuzi wa watu. Haya yanajiri baada ya wiki nzima ya maandamano yaliyioongoizwa na vijana kutoka […]

BUNGE LAIDHINISHA WANAJESHI VICHOCHORONI

Bunge la kitaifa limeidhinisha hatua ya jeshi la KDF kutumwa ili kushirikiana na maafisa wa polisi kurejesha utlivu nchini baada maafa yaliyosabibishwa na maandamano ya kupinga mswada wa fedha. Mswada huo ambao umewasilishwa na kiongozi wa walio wengi katika bunge hilo Kimani Ichung’wa na kupigiwa kura na wabunge, saa chache baada ya Waziri wa ulinzi […]

KARUA: MNAWATUMIA WANAJESHI VIBAYA

Muda mfupi baada ya bunge kuidhinisha kutumkwa kwa wanjeshi kwenye operesheni ya kurejesha utulivu nchini, kinara wa chama cha Narc Kenya Martha Karua ameshutumu hatua hiyo, akisema serikali inawatumia wanajeshi kulinda maslahi ya baadhi ya viongozi. Katika taarifa kwa wanahabari, Karua aidha ameshutumu visa vya maafisa wa polisi kutumia nguvu kupita kiasi kuwakabili waandamaji. Aidha, […]

KWA NINI RUTO ASIIDHINISHE MSWADA WA FEDHA – AHMEDNASIR

Wakili Ahmednasir Abdullahi anasema Rais William Ruto hafai kuidhinisha Mswada wa Fedha wa 2024.Katika taarifa , Ahmednasir amesema ni lazima Rais aurejeshe bungeni kwa marekebisho na kuongeza kuwa Ruto anahitaji kutafuta njia ya kuondoa ushuru unaowakandamiza wakenya ulioko katika Mswada huo. Aidha amebainisha kuwa ni wakati wa Rais Ruto kusikiliza wito kutoka kwa Wakenya wa […]

MCHAMBUZI WA MITANDAO YA KIJAMII GABRIEL OGUDA AACHILIWA

Mchambuzi maarufu wa mitandao ya kijamii Gabriel Oguda ameachiliwa baada ya kuripotiwa kutekwa nyara na watu wanaoaminika kuwa maafisa wa polisi. Kuachiliwa kwake kumethibitishwa na mtumiaji wa X Nyandia Gachago Jumatano ambaye amesema Oguda Yuko salama” baada ya kushiriki picha inayoonyesha watu wanne kati yao Oguda ambaye alitoweka tangu siku ya Jumanne asubuhi. Kukamatwa kwake […]

MAWAKILI WAELEKEA MAHAKAMANI KUMZUIA RAIS RUTO KUSAINI MSWADA WA FEDHA KUWA SHERIA

Timu ya mawakili imewasilisha ombi la kutaka kumzuia Rais William Ruto kuidhinisha Mswada tata wa Fedha wa 2024 kuwa sheria. Katika kesi hiyo, walalamishi hao wanahoji kuwa “hakujakuwa na “ushiriki wa umma halali au unaofaa kuhusu Mswada wa Fedha wa 2024 ambao Bunge la Kitaifa liliidhinisha jana Jumanne huku kukiwa na maandamano ya ghasia nchini. […]

BUNGE LAKUTANA KUIDHINISHA KUTUMWA KWA KDF

Bunge la Kitaifa limeandaa kikao maalum kuidhinisha ombi la Baraza la Ulinzi la kupeleka Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF) huku kukiwa na maandamano ya kupinga Mswada wa Fedha kote nchini. Kulingana na Waraka wa Amri ya Ziada iliyopangwa leo, hatua hiyo itaambatana na Kifungu cha 241 cha Katiba kinachohitaji kuidhinishwa na Bunge kabla ya […]

MKUTANO WA KILELE WA UWEKEZAJI NYANZA WAAHIRISHWA

Kongamano la kimataifa la uwekezaji la Nyanza lililokuwa likitarajiwa kufanyika kuanzia Ijumaa limeahirishwa. Waandalizi wa hafla hiyo ya kikanda wanasema imepangwa upya ili kukabiliana na hali ya sasa nchiniTarehe mpya ya kongamano hilo itatangazwa baadaye. Rais William Ruto na kinara wa upinzani Raila Odinga walitarajiwa kuhudhuria mkutano huo uliolenga kuwaleta pamoja wataalamu mbalimbali kutoka kaunti […]

UMOJA WA MATAIFA WAKASHIFU MAUAJI YA WAANDAMANAJI KENYA

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameeleza wasiwasi wake kuhusu ghasia zilizoshuhudiwa wakati wa maandamano ya kupinga Muswada wa Fedha wa 2024 humu Kenya. Katika taarifa Guterres amezitaka mamlaka za Kenya kuandaa maandamano ya amani ili kuepusha madhara na vifo vya watu zaidi. Imetayarishwa na Janice Marete