WATU 13 WAUAWA KATIKA MAANDAMANO

Watu 13 wamedhibitishwa kufariki dunia na wengine 150 kujeruhiwa katika maandamano huku mashirikia ya kutetea haki za binadamu yakiendeleza shutumu dhidi ya serikali kwa kutumia nguvu kupita kiasi. Chama cha mawakili nchini LSK kikiongozwa na rais wao Faith Odhiambo kimeahidi kuwasaidia waadhiriwa wote kutafuta haki kwa wapendwa wao. Hussein Khalidi mkurugenzi wa haki Afrika amesema […]

TUUNGANE TUJENGE AFRIKA;RAIS RUTO ASEMA

Rais William ruto anaongoza kikao cha mageuzi katika umoja wa afrika mjini Naivasha kaunti ya NakuruKwa mujibu war ais Ruto pana haja ya mataifa ya afrika kushirikiana kuboresha majukumu ya muungano wa afrika AU kwa manufaa ya wananchi. Imetayarishwa na Janice Marete

WATU SITA WAHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 15 MAUAJI YA JUJA GEORGE THUO.

Watu sita waliopatikana na hatia katika mauaji ya aliyekuwa mbunge wa Juja George Thuo wamehukumiwa kifungo cha miaka 15 jela. Mahakama pia imebainisha kuwa wana haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo.Sita hao wamepatikana na hatia ya kumuua mbunge huyo wa zamani mwaka wa 2013 katika eneo moja la burudani mjini Thika Imetayarishwa na Janice Marete

WAKO WAPI WANAHARAKATI MLIOWAKAMATA? OPIYO AULIZA POLISI

Kiongozi wa wachache katika bunge la kitaifa Opiyo wandayi amewalaumu maafisa wa polisi kwa kukamatwa kwa wanaharakati wanaodaiwa kuongoza maandamano ya kupinga mswada wa fedha. Akizungumza katika bunge la kitaifa katika kikao kinachoendelea kwa sasa Opiyo ameilaumu serikali kwa kukamatwa kwa mwanabloger Gabriel Oguda kutokana na msimam o wake dhidi ya mswada wa fedha. Opiyo […]

MBAPPE APATA NAFUU

Kocha wa Ufaransa Didier Deschamps  amefichua kwamba Kylian Mbappe anaimarika kila siku” lakini hakuthibitisha kama nahodha wake angeanza mechi ya mwisho ya kundi la Euro 2024 leo dhidi ya Poland. Mbappe hakushiriki katika sare ya 0-0 na Uholanzi Ijumaa iliyopita mjini Leipzig baada ya kuvunjika pua kwenye ushindi wa 1-0 wa timu yake dhidi ya […]

CITY THUNDER WANGURUMA

Licha ya kuwa nafasi moja waingie katika fainali ya Ligi Kuu ya Kitaifa ya Mpira wa Kikapu ya Wanaume, kocha mkuu wa Nairobi City Thunder Brad Ibs amekiri kwamba haikuwa rahisi kuwapita Equity Dumas katika mchujo wa nusu fainali. Thunder, ambao hawajashindwa msimu huu, wanaingia fainali baada ya ushindi wa 2-0 katika mchujo wa nusu […]

OMALLA ATAJWA KWA KIKOSI CHA COSAFA

Mfungaji bora wa Ligi Kuu ya FKF 2023/24 Benson Omalla ni miongoni mwa wachezaji ambao wamefuzu katika timu ya mwisho ya Kenya ya U23 inayosafiri kwa  Kombe la COSAFA linalotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 26 hadi Julai 7, 2024, nchini Afrika Kusini. Mshambulizi huyo wa Gor Mahia mwenye umri wa miaka 22 alifunga mabao 19 na […]

BARABARA ZINAZOELEKEA BUNGENI ZAFUNGWA

Jiji la nairobi na miji mingine ya humu nchini inatarajia maandamano makubwa ya kupinga mswada wa fedha huiku barabara kadhaa zinazoelekea kwenye majengo ya Bunge la kitaifa zikizifungwa na maafisa wa usalama kushika doria. Barabara ya parliament road na ile ya city way, miongoni mwa zingine, zimefungwa kwa trafiki ya magari na ufikiaji wa wanaotembea […]

KITAELEWEKA BUNGENI LEO

Bunge la Kitaifa leo linatarajiwa kupiga kura kuunga au kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2024 ambapo wabunge watapiga kura kipengele moja baada ya kingine Pande za Kenya Kwanza na Azimio zinajiandaa kutetea marekebisho mbalimbali ambayo yamependekeza kwenye Mswada huo huku mrengo wa Azimio wakihapa kuangusha mswada mzima. Imetayarishwa na Janice Marete

KENYA YATEULIWA RASMI NA MAREKANI KAMA MSHIRIKA MKUU ASIYE WA NATO

Rais wa Marekani Joe Biden ameteua rasmi Kenya kuwa mshirika mkuu asiye wa NATO. Uteuzi huo unajiri wiki chache baada ya ziara ya kitaifa ya Rais William Ruto nchini Marekani. Ni wakati wa ziara ya serikali ambapo Biden ametangaza nia yake ya kuwa na Kenya kama mshirika mkuu asiye wa NATO. NATO ambayo inawakilisha Shirika […]