HOMA BAY YAANZISHA MIPANGO YA KUFUNFUA VIWANDA HUKO KARACHUONYO

Serikali ya kaunti ya Homa Bay inatayarisha mpango mkuu wa kuanzisha viwanda katika Eneo Maalum la Kiuchumi la Riwa katika eneo bunge la Karachuonyo. Mpango huo unaandaliwa baada ya uchunguzi wa hali ya hewa kufanyika ili kuiwezesha serikali kuweka ramani na kutambua maeneo ambayo viwanda vitaanzishwa. Serikali ya kaunti hiyo inashirikiana na mashirika mengine, Mamlaka […]

RAIA AWAJERUHI WATATU KWA RISASI

Watu watatu wamepigwa risasi na kujeruhiwa na raia mmoja wakati wa maandamano jijini Mombasa. Imearifiwa kuwa raia huyo amekasirishwa na waandamanaji waliokuwa wamelemaza shughuli za biashara ndipo akaamua kuwafyetulia risasi kwenye barabara ya Nyerere. Wakati wa maandamano hayo, mkahawa mmoja wa kifahari umevamiwa, huku waandamanaji wakimsaka raia huyot. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAANDAMANAJI WACHOMA MAGARI MOMBASA

Kundi moja la waandamanaji jijini Mombasa limeteketeza takribani magari matano wakati wa maandamano huku wakiimba nyimbo za kumtaka rais William Ruto aondoke mamlakani. Hata hivyo, kikosi cha wazima moto kimewasili na kuanzisha juhudi za kuzima moto huo, huku kiini cha kuteketeza magari hayo ikiwa bado hakijulikani.. Maandamano yameendelea katika maeneo kadhaa ya Mombasa, ikiwemo Mwembe […]

‘MAJENEZA YA MAANDAMANO’ NAIROBI

Waandamanaji wameingia na takribani majeneza 10 katikati mwa jiji la Naiorbi, baadhi yao yakiwa yamefunikwa kwa bendera za taifa. Waandamanaji hao wameyaweka majeneza hayo kwenye foleni, na baadhi yao wakiyafungua majeneza hayo. Hata hivyo, maafisa wa polisi wameyachukua na kuyapakia katiika lori moja jeupe, na haijulikani ni wapi wameyapeleka. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

KNUT YAMTAKA RAIS RUTO KUSHUGHULIKIA GEN-Z

Chama cha Kitaifa cha Walimu (KNUT), tawi la Kisumu, kimeitaka serikali kuharakisha kushughulikia madai ya Gen- Z kukomesha maandamano na kurejesha hali ya kawaida huku shule zikifunguliwa baada ya likizo fupi. Akihutubia wanahabari, David Obuon, Katibu Mtendaji wa KNUT tawi la Kisumu, amesema kuwa shule nyingi za mijini zinategemea usafiri wa umma, na kutokana na […]

BARABARA ZOTE ZINAZOELEKEA IKULU YA NAIROBI ZAFUNGWA

Barabara zote zinazoelekea Ikulu ya Nairobi, zimesalia kufungwa huku maandamano yakianza katika baadhi ya miji nchini huku Milango yote kuu ya ikulu ya nairobi ikisalia kufungwa. Imetayarishwa na Janice Marete

KENNEDY ALIUAWA NA POLISI RONGAI WAKATI WA MAANDAMANO

Mwanapathologia wa serikali Peter Ndengwa aliyeufanyia mwili wa Kennedy Onyango upasuaji amebaini kuwa kennedy aliaga dunia kutokana na jeraha mbaya la risasi. Mtoto huyo mwenye umri wa miaka 12 ambaye alipoteza Maisha yake wakati wa maandamano siku ya alhamisi eneo la Rongai kaunti ya Kajiado alipigwa risasi wakati wa maandamano hayo alipokuwa akielekea kwa rafikiye kuomba kitabu. […]

WAKENYA ANA KWA ANA NA ‘UKOSEFU’ WA MSWADA

Wakenya sasa watakosa maendeleo kutokana na matumizi madogo ya bajeti ya mwaka huu 2024/2025 katika serikali kuu na ile ya kaunti baada ya mswada wa kifedha kutupiliwa mbali, hii ni kwa mujibu wa ripoti kutoka ofisi ya bajeti ya kitaifa.   Hata hivyo, hili linaongezea hasara ambayo taifa hupata kila mwaka kutokana na ufisadi ambayo […]

TEKELEZENI AFCFTA, AFRIKA YASHAURIWA

Nchi za Afrika zimetakiwa kutoa mipango kazi na mikakati ya kitaifa ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa Eneo la Biashara Huria la Afrika (AfCFTA) na maingiliano ya kiuchumi baina ya nchi hizo. Wito huo umetolewa katika Jukwaa la Majadiliano ya Kitaifa kuhusu Maendeleo ya Mkakati wa Utekelezaji wa eneo la biashara huria nchini Ethiopia lililofanyika […]

MASWALI YA DCI KWA KETER

Mbunge wa zamani wa Nandi Hills Alfred Keter amehojiwa wa makachero wa idara ya upelelezi DCI katika makao makuu ya idara hiyo, akifichua kwamba ametakiwa kuweka wazi uhusiano uliopo baina yake na Rais mstaafu Uhuru Kenyatta na Naibu Rais Rigathi Gachagua. Akizungumza na wanahabari baada ya kuhojiwa, Keter aidha, amesema ameulizwa kuhusiana na Sakata za […]