EMERGING STARS WACHARAZA ZIMBABWE 2-0

Emerging stars jana walirejea katika njia za ushindi katika michuano ya Cosafa mwaka huu inayoendelea ambapo waliandikisha ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Zimbabwe katika uwanja wa Wolfson mjini port Victoria Afrika Kusini Osteen Odhiambo alifunga mbao la kwanza dakika ya 54 naye benson Omala akaongeza la pili dakika ya 73. Emerging starrs walimaliza katika […]

TOLEO LA TATU LA NAIROBI CITY MARATHON LIMEAHIRISHWA

Shirikisho la riadha nchini na kamati ya maandalizi ya nairobi city marathoni zimetangaza kuahirishwa kwa toleo la tatu la mashindano hayo Kwa mujibu wa kamati andalizi mbio hizo zimesitishwa kwa sababu zisizoweza kuepukika na kwamba hafla hiyo itafanyika septemba tarehe nane mwaka huu Imetayarishwa na Janice Marete

SERIKALI IMEWASALITI WAKENYA; OMANGA MILLICENT ASEMA

Aliyekuwa Seneta mteule Millicent Omanga sasa anasema kuwa kuongeza mishahara ya maafisa wa serikali wakati huu sio nzuri. Katika taarifa yake Omanga amesema kutokana na msukosuko wa sasa wa kutaka mishahara hiyo ipunguzwe, ni sawa na kuwasaliti Wakenya. Omanga aidha amesema kuwa Wakenya hawafai kudanganywa na viongozi kila mara huku akisisitiza kwamba wanachotaka wananchi kwa […]

SENETA MADZAYO AKATAA NYONGEZA YA MSHAHARA

Kiongozi wa wachache katika Seneti Stewart Madzayo sasa anasema hataki nyongeza yoyote ya mishahara. Akizungumza katika ukumbi wa Bunge leo Jumatano, Madzayo amekataa nyongeza hiyo iliyopendekezwa huku akiwa na matumaini maseneta wenzake watafuata nyayo zake akisema sio wakati mzuri wa nyongeza. Imetayarishwa na Janice Marete

MATUMAINI YAPO KWA KENYA KUONGEZA MAPATO

Kenya bado inaweza kuongeza mapato zaidi kutokana na ushuru wa forodha na kusaidia ukuaji wa viwanda vyake vya ndani licha ya kuanguka kwa Mswada wa Fedha wa 2024. Hii inafuatia uamuzi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuipatia Kenya matakwa yake kuhusu mapendekezo kadhaa ya kutoza ushuru wa juu zaidi wa bidhaa zilizomalizika, huku ikiruhusu […]

MENEJA WA UWEKEZAJI KUJUA HATIMA YAKE LEO

Jaji wa Mahakama ya Juu Nixon Sifuna leo hii anatarajiwa kutoa uamuzi wake katika rufaa iliyowasilishwa na aliyekuwa meneja wa uwekezaji Francis Moturi baada ya kupatikana na hatia katika kesi inayomkabili ya kusababisha hasara ya shilingi bilioni 1.2 katika wizara ya NSSF. Mahakama ya Hakimu Mkazi ilimpata na hatia mnamo Januari 2022 na kumhukumu kifungo […]

GEN-Z MLIKENI SERIKALI ZA KAUNTI;ELSIE MUHANDA ASEMA

Mwakilishi wa kike katika kaunti ya Kakamega Elsie Busihile Muhanda amewataka vijana kuanza kumlika serikali za kaunti ili kubaini iwapo viongozi wanatekeleza miradi ya maendeleo kama walivyoahidi wakati wa kampeni. Muhanda aidha ameonyesha kurithishwa na juhudi za vijana wanaoendeleza maandamano ili kushinikiza serikali kutekeleza ahadi zake kwa wananchi. Imetayarishwa na Janice Marete

WANAHARAKATI WA KUTETEA HAKI ZA BINADAMU WAPENDEKEZA FEDHA ZAIDI KWA IDARA YA MAHAKAMA

Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu na wasimamizi wa mashirika ya kijamii eneo la magharibi wametoa wito kwa serikali kuongeza mgao wa fedha katika idara ya mahakama. wanahakati hao wanasema kuwa hatua hiyo itawezesha kutenga fedha za kufanikisha kesi za dhuluma za kijinsia kwa haraka ili familia husika zipate haki. Imetayarishwa na Janice Marete

DCI WACHUNGUZA MAUAJI YA NANCY WANJOGU NYERI

Maafisa wa idara ya upelelezi DCI wanachunguza mauaji ya Nancy Wanjogu mwanamke mwenye umri wa miaka 26 ambaye mwili wake umepatikana katika nyumba yake kijiji cha Kwamuya,Karatina, Kaunti ya Nyeri. Kulingana na Polisi mwili huo ulikuwa na majeraha mabaya wakati ulipogunduliwa ,kakake marehemu amewaambia polisi kwamba alipokea simu kutoka kwa marehemu kwamba maisha yake yalikuwa […]

WAADHIRIWA WA MAANDAMANO KAKAMEGA WAOMBA MSAADA

Zaidi ya watu kumi waliojeruhiwa wakati wa maandamano katika kaunti ya Kakamega wametoa wito kwa gavana wa kaunti hiyo Fernadez Barasa kuwasaidi ili madaktari waweze kuwaondolea risasi mwilini kwa kuwa hawawezi kumudu gharama ya matibabu. Imetayrishwa na Janice Marete