NDANGIRI ANAAPA KUNYAKUA TAJI LA PILI LA KENYA LA U-20

Mshindi wa medali ya shaba ya mbio za mita 10,000 kwa Waafrika 2023, Stephen Ndangiri, ameapa kutwaa taji la dunia la mbio za wat5u walio na umri chini ya miaka 20 U20 mjini Lima, Peru, michuano hiyo itakapoanza Taji pekee la awali la Kenya katika hafla hii lilitoka kwa Haristone Wanyonyi, ambaye alitumia 42:10.84 mnamo […]

KISA CHA PILI CHA MPOX CHAGUNDULIWA KENYA

Kisa cha pili cha ugonjwa wa Mpox kimegunduliwa humu nchini, Waziri wa afya Deborah Mulongo akisema kisa hicho kimegunduliwa baada ya sampuli kutoka kwa dereva wa trela katika mpaka wa Kenya na Uganda mjini Malaba kaunti ya Busia kufanyiwa vipimo. Amesema mgonjwa huyo amewekwa karantini katika kituo kimoja cha afya kaunti ya Busia ambako anatibiwa. […]

LIPA HUSTLER FUND AU ‘USALIMIWE’, OPARANYA

Huenda wakenya ambao wamefeli kulipa mkopo wa Hustler Fund wakajipata pabaya baada ya Waziri wa vyama vya ushirika na biashara ndogo ndogo Wycliffe Oparanya kutangaza msako dhidi yao. Akizungumza jijini Nairobi, Oparanya amesema wizara yake imeanzisha mchakato wa kubuni mfumo utakaofanikisha kuwanasa wakenya hao, na kupongeza hazina hiyo akisema ililenga kubuni nafasi za ajira. Wakati […]

WANAFUNZI WALALAMIKIA KATEGORIA TATA

Hazina ya kufadhili elimu ya juu imepokea malalamishi kutoka kwa wanafunzi zaidi ya 10,000 wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu, wakisema wamewekwa katika kategoria ambazo haziwiani na mapato ya familia zao. Mkurugenzi mkuu wa hazina hiyo George Munari amesema kuwa zoezi la kukagua malalamishi hayo litachukua muda wa wiki tatu. Aidha, ametoa wito kwa usimamizi wa […]

WAWAKILISHI WADI MERU WAMKANA MWANGAZA

Baadhi ya wawakilishi wadi katika kaunti ya Meru wanamtaka gavana wa kaunti hiyo Kawira Mwangaza kuondoka kwenye afisi za kaunti hiyo hadi kesi aliyowasilisha mahakamani kupinga kutimuliwa kwake itakaposikilizwa na kuamuliwa. Wakiongozwa na kiongozi wa walio wengi katika bunge la kaunti hiyo Patrick Mutuma, wawakilishi hao wameshikilia kwamba hawamtambui Mwangaza kuwa gavana wao. Wakati uo […]

MAHAKAMA YALENGA KURAHISISHA HAKI

Jaji mkuu Martha Koome amezindua majopokazi 26 yatakayohakikisha uarahisi katika upatikanaji wa haki, hatua hiyo ikilenga kuhakikisha wananchi hasa walio maeneo ya mashinani wanapata huduma za kisheria kwa urahisi. Kwa mujibu wa Koome, mikakati iliyowekwa tayari imezaa matunda, zaidi ya kesi 15,000 zikitatuliwa. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

WAZAZI WAWATAKA WALIMU KURUDI SHULENI

Muungano wa kitaifa wa wazazi umewataka walimu kufutilia mbali mgomo wao ambao umeratibiwa kuanza wiki ijayo shule zitakapofunguliwa kwa muhula wa tatu. Mwenyekiti wa kitaifa wa muungano huo Silas Obuhatsa, amehofia kudhoofika kwa masomo wakati huu ambapo wanafunzi wanafaa kujiandaa kwa mitihani ya kitaifa. Aidha, ameitaka miungano ya walimu KNUT na KUPPET kuangazia upya uamuzi […]

KeNHA KUFUNGA BARABARA ENEO LA GITARU, KIAMBU

Shughuli za usafiri zimeratibiwa kutatizika kwenye barabara kuu ya Nakuru kuelekea Nairobi Jumatano ijayo, baada ya mamlaka ya barabara kuu KeNHA kutangaza kwamba itafunga barabara hiyo katika eneo la Gitaru kaunti ya Kiambu ili kuruhusu ujenzi wa Gitaru interchange. Kupitia taarifa, KeNHA imesema magari yanayotokea upande wa Nakuru yatachukua barabara ya Regen/Magara na kujiunga na […]

MIAMBA WA RAGA KENYA KWENYE NUSU FAINALI RAGA

Shule ya upili ya All Saints ya Embu imeratibiwa kumenyana na wenzao Kitondo katika semi fainali za raga ya wachezaji 15 kila upande katika mashindano yanayoendelea ya shirikisho la shule za upili ukanda wa Afrika nchini Uganda. All saints ambao ndio mabingwa wa Kenya, walifuzu kwenye fainali baada ya kumaliza kileleni mwa kundi lao bila […]

WANYONYI, MORAA WATIA FORA DIAMOND LEAGUE

Mshindi wa dhahabu ulimwenguni katika mbio za mita 800 za Olimipiki Emmanuel Wanyonyi ametia fora na kuibuka mshindi katika mashindano ya Diamnond League kwenye mbio hizo jana usiku nchini Uswizi, na kumpiku mshindani wake wa siku nyingi Marco Arop wa Canada. Wanyonyi aliandikisha muda wa dakika 1. Sec 41.11, ukiwa ndio muda wa kasi zaidi […]