MUDAVADI; NAUNGA MKONA HAZIMA YA RAILA 100%

Waziri mwenye mamlaka makuu Musalia Mudavadi amesema kuwa yuko tayarai kumunga mkono kinara wa ODM Raila Odinga katika hazima yake ya kuwania wadhifa wa mwenyekiti wa umoja wa afrika AUC. Kwa mujibu wa Mudavadi Odinga hawakilishi tu taifa la kenya bali bara nzima la afrika kwa kuwa anajumuisha matarajio ya mamilioni ya waafrika wanaotafuta bara […]

MWANIKI ATOLEWA NJE

Mwendesha baiskeli Benson Mwaniki ameondolewa kwenye Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya Paris 2024, baada ya kuvunjika bega na uti wa mgongo katika ajali mbaya wiki iliyopita. Mwaniki, ambaye alikuwa rubani wa mwendesha baiskeli Kennedy Ogada, anahitaji angalau wiki sita kupata nafuu baada ya kuangushwa na gari walipokuwa wakienda mazoezini huko Compiegne, Ufaransa. Hata hivyo, […]

ADAM AANDIKA HISTORIA

Mwanalima Adam ameandikisha historia kwa kuwa Mkenya wa kwanza kucheza Ligi ya Taifa ya Wanawake (NWSL) nchini Marekani, akiwakilisha timu yake mpya, Kansas City Current. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 aliingia uwanjani katika dakika ya 65 akichukua nafasi ya Claire Hutton wakati tayari walikuwa chini kwa mabao 3-1. Ingawa hajafurahishwa na matokeo hayo, […]

WANJALA AJIUNGA NA ATHLETIC CLUB

Beki wa Kenya anayeimarika kwa kasi, Amos Wanjala amejiunga na klabu ya Athletic Club Torrellano inayoshiriki ligi ya daraja la tano nchini Uhispania. Wanjala umaarufu wake umekuwa ukiongezeka tangu mwaka jana alipohamia Uhispania pamoja na Aldrine Kibet na Alvin Kasavuli pamoja na Vijana wengine kadhaa wa Kenya. Watatu hao walijiunga na Nastic Sports Academy kufuatia […]

KINERO NDO KOCHA WA MOMBASA UNITED.

KLABU iliyopewa jina jipya, Mombasa United imemteua Swaleh Kinero Ali kama kocha mkuu mpya. Kinero anarejea katika usimamizi baada ya kuinoa Harambee Sand Stars katika Michezo ya Ufukweni ya Afrika Juni mwaka jana. Alikuwa sehemu ya timu ya Coast Talanta Hela iliyopewa sifa kwa kuibua vipaji vipya kama Amos Wanjala, William Gitamu, Abdulhafidh Abdallah, na […]

VIONGOZI WA ODM KAKAMEGA WAMSIFU RUTO

Viongozi wa ODM kaunti ya Kakamega wamemtakia kiongozi wa chama hicho Raila Odinga ushindi katika kinyanganyiro cha mwenyekiti wa umoja wa afrika AUC. Wakiongozwa na gavana wa kaunti hiyo ya Kakamega Fernadez Barasa viongozi hao wamemlimbikizia sifa rais william Ruto kwa kuunga mkono hazima ya Odinga kuchukua wadhifa huo. Imetayarishwa na Janice Marete

VIJANA ZAIDI YA 200 KUJIUNGA NA CHUO CHA KIUFUNDI KITALE HUKO TRANSNZOIA

Vijana zaidi ya 200 kutoka wadi ya Waitaluk katika kaunti ya Transnzoia wamehamasishwa na kurtatibiwa kujiunga na chuo cha kiufundi kitale ili kupata ujuzi wa taaluma mbalimbali. Kwa mujibu wa mwakilishi wa wadi ya waitaluk Lusweti Furaha mpango huo unalenga kusuluhisha tatizo la ukosefu wa ajira nchini huku akikahidi kuwa vijana hao watakapohitimu watapokezwa vifaa […]

AACHILIWA BAADA YA KUFUNGWA KIMAKOSA MIAKA 13

Shangwe na nderemo zilijaa nyumbani kwa Peter Githinji Kioi, mkazi wa kijiji cha Kiangothe Kirinyaga ya Kati, aliporejea nyumbani baada ya kukaa gerezani kwa miaka 13. Githinji, ambaye alikuwa akitumikia kifungo cha maisha jela katika Magereza ya King’ong’o, aliachiliwa baada ya kufanikiwa kukata rufaa dhidi ya hukumu yake. Masaibu ya Githinji yalianza mkewe alipomshtumu kwa […]

MWANAMKE AZIKWA AKIWA HAI SHIMO LA MGODI WA DHAHABU LIKIPOROMOKA HUKO SIAYA

Mwanamke mwenye umri wa miaka 32 amefariki baada ya shimo la kuchimba dhahabu kuzamia na kumfunika akiwa hai katika kijiji cha Uradi, Kaunti ya Siaya. Kulingana na Chifu Msaidizi wa eneo hilo Grace Otieno, mwanamke huyo kwa jina Rosemary Anyango alikuwa pamoja na wengine wanne alipokumbana na mauti. Anasema kuwa wanawake hao walikuwa katika shughuli […]