WANARIADHA WANAZIDI KUMUOMBELEZA REBBECCA

Wanariadha wamemuomboleza mwendazake Rebecca Cheptegei kama mwanariadha mwenye kipawa ambaye alitazamiwa kuwa mmoja wa wanariadha bora wa mbio za masafa marefu katika ukanda huu. Wakiongozwa na mshirika mwenza mazoezini James Kirwa, walisema marehemu aliyefariki akiwa na umri wa miaka 33 alikuwa mkarimu na amewasaidia wakimbiaji wengine kifedha. Cheptegei, ambaye alishiriki katika Michezo ya Olimpiki ya […]

TUKO TAYARI KWA OLIMPIKI

Makamu wa rais wa chama cha riadha nchini Paul Mutwii anasema wanariadha wa chini ya umri wa miaka 20 walioshiriki Mashindano ya Dunia ya U-20 mwaka huu huko Lima, Peru watakuwa tayari kwa Michezo ya Olimpiki ya Los Angeles mnamo 2028. Vijana hao walirejea nchini mapema leo baada ya kuvuna medali saba; tatu za dhahabu, […]

TUEKEZE ZAIDI

Mshindi mpya wa medali ya fedha katika Michezo ya Olimpiki ya Walemavu Samson Ojuka ametoa wito wa kuwekeza zaidi katika mashindano hayo ikiwa Kenya inataka kupelekana sako kwa bako na miamba wa dunia. Ojuka alishinda medali ya fedha katika Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya Paris mnamo Jumanne katika fainali yaurukaji kwa urefu kitengo cha […]

MADAKTARI, WAUGUZI WATISHIA MGOMO WA KITAIFA

Huenda wakenya wanaosaka huduma za kimatibabu katika hospitali za umma wakajipata kwenye hali ngumu kwa mara nyingine tena, baada ya muungano wa madaktari KMPDU kutoa makataa ya siku 14 kwa serikali iwalipe malimbikizi ya mishahara yao la sivyo wagome. Katika kikao na wanahbari, katibu mkuu wa KMPDU Davji Atellah ameonyesha masikitiko kuhusiana na kucheleweshwa kwa […]

MWAURA: SERIKALI KUKAGUA MIRADI KOTE NCHINI

Serikali imetengaza kuendesha zoezi la kukagua miradi yote nchini iliyoanziasha, msemaji wa serikali Isaac Mwaura akifichua haya baada ya kuibuka ripoti kwamba kuna miradi ambayo imtelekezwa huku nyingine ikikabiliwa na Sakata za ufisadi. Katika kikao na wanahabari jijini Nairobi, Mwaura amesema kwamba maafisa kutoka afisi ya rais watafanya ukaguzi wa kina katika maeneo yote ya […]

FAMILIA YA CHEPTEGEI YAWALAUMU POLISI

Familia ya mwanariadha wa Uganda Rebecca Cheptegei sasa inailaumu serikali kwa kifo cha mwanariadha huyo ambaye ameaga dunia mapema leo, wakisema kabla ya kushambuliwa, waliwasilisha malalmishi ya kutishiwa kwake na mshukiwa kwa idara ya upelelezi DCI ila hakuna hatua iliyochukuliwa. Wakionggozwa na babake Joshua Chaptegei, wamesema kifo cha mwanao ni pigo kwao kama familia, wakisema […]

RAILA ANGALI MCHEZONI, ODM

Katibu mkuu wa chama cha ODM Edwin Sifuna amekariri kwamba kiongozi wa chama hicho Raila Odinga hajastaafu kutoka ulingo wa siasa, akipuuzilia mbali taarifa zilizodai kwamba Odinga amestaafu. Kupitia taarifa, sifuna amezitaja habari hizo kuwa zenye nia mbaya na zenye nia ya kuwavunja mioyo wafuasi wa ODM. Aidha, amewataka wafuasi kuzipuuza taarifa hizo. Imetayarishwa na […]

MWAKILISHI WA KIKE KAUNTI YA TRANSNZOIA LILIAN SIYOI APENDEKEZA MASOMO YA BURE KWA WANAFUNZI WA SHULE ZILIZOKO KATIKA MAZINGIRA YASIYO RASMI

Wanafunzi wanaosoma katika shule zilizo maeneo yasiyo rasmi huenda wakanufaika na masomo ya bure iwapo pendezo la Mwakilishi wa kike katika kaunti ya Transnzoia Lilian Siyoi Chebet la kutengewa hazina maalum itakayokithi mahitaji yao yote litaithinishwa. Kwa mujibu wa Siyoi hali ya uchumi wa taifa kwa sasa hairuhusu kuwepo kwa masomo ya bure kwa kila […]

KATIBU MKUU WA KUPPET AKELO MISORI AKASHIFU WANACHAMA WANAOMSHUTUMU KWA USALITI

Katibu Mkuu wa Muungano wa sekondari na vyuo vya kadri (KUPPET) Akelo Misori ameshikilia kuwa kusitishwa kwa mgomo wa walimu siku ya Jumatatu sio uamuzi wake mwenyewe, bali uamuzi wa chama cha wafanyakazi. Misori, ambaye ameshutumiwa kwa usaliti na baadhi ya wanachama wakuu wa KUPPET amesema wanachama hao ni wanafiki. Ameongeza kuwa walisitisha mgomo huo […]