GAVANA LENOLKULAL APINGA HUKUMU

Gavana wa zamani wa Samburu Moses Lenolkulal amekata rufaa dhidi ya hukumu aliyopewa na mahakama wiki jana baada ya kupatikana na hatia ya ufisadi inayohusu shilingi milioni 83.4 alipokuwa mamlakani. Kupitia kwa mawakili wake, Lenolkulal anasema kulikuwa na dosari katika hukumu hiyo na kumshutumu hakimu Thomas Nzioka kwa kukosa kufanya uchunguzi wa kina kwenye ushahidi, […]

GATUSSO AREJEA KIZIMBANI

Mchezaji wa zamani wa Harambee Stars Collins Okoth Ougo almaarufu Gattuso leo alifikishwa mahakamani pamoja na mshtakiwa mwenzake Silvia Aoko kuhusu mauaji ya mtoto mdogo katika mtaa wa Lucky Summer Estate, Ruaraka, Nairobi. Wawili hao walifikishwa mbele ya Hakimu Alexander Muteti katika Mahakama ya Milimani lakini hawakujibu mashtaka hayo. Upande wa mashtaka ulithibitisha kuwa washukiwa […]

USHINDI UMEIMARISHA KIKOSI

Kocha mkuu wa KCB RFC kikosi chao cha raga ya wachezaji saba kila upande Andrew Amonde anasema ushindi wa Kabeberi Sevens umeongeza ushindani mzuri miongoni mwa wachezaji wake wanapoelekea kwa mikondo miwili ya mwisho ya msururu wa kitaifa wa raga ya wachezaji saba. Amonde alisema kuwa kila mchezaji ana ari na anataka kuwa sehemu ya […]

KISIA AINGIA IMPALA

Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Kenya raga ya wachezaji saba kwa wanaume, Louis Kisia anatarajiwa kuteuliwa kocha mkuu mpya wa Impala Club. Kisia alijiuzulu kama kocha mkuu wa Strathmore Leos mwezi Machi mwaka huu na tangu wakati huo amekuwa na kazi ngumu na timu ya taifa lakini sasa atarejea katika raga ya klabu […]

HAKI YETU

Familia ya mwanariadha wa Uganda, Rebecca Cheptegei, ambaye alishiriki mbio za mita 10,000 kwenye michezo ya Olimpiki ya mwaka huu jijini Paris, Ufaransa imetaka hatua kali na za haraka zichukuliwe dhidi ya wahusika wa shambulio lililosababisha asilimia 75 ya majeraha ya moto mwilini mwake kufuatia madai ya mzozo kati yake na mpenzi wake Jumapili iliyopita. […]

RAHEEM ASHABIKIA KUINGIA ARSENALI

Baada ya kuhama kutoka Chelsea kwenda Arsenal siku ya mwisho ya ruhusa ya uhamisho, Raheem Sterling anahisi kwamba kuhama kutoka Magharibi mwa London hadi kaskazini mwa London ni hatua sahihi katika maisha yake ya soka. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza alifanikiwa kukamilisha uhamisho wa mkopo wa msimu mzima kutoka Chelsea, na hivyo kuhitimisha biashara […]

VYUO VIKUU KUANDAMANA KUPINGA MFUMO WA UFADHILI WA ELIMU YA JUU

Viongozi wa wanafunzi kutoka vyuo mbali mbali humu nchini wameendelea kuishinikiza serikali kubadilisha au kufutilia mbali kabisa mfumo wa ufathili wa elimu ya juu la sivyo watalemaza shughuli za masomo katika vyuo vikuu. Wanafunzi hao wanapendekeza kupunguzwa kwa riba inayotozwa kwenye mikopo ya elimu ya juu kutoka asilim ia 4 hadi asilimia 2. Iwapo matakwa […]

KAMATI YA ULINZI YA BUNGE YAPOKEA MALALAMISHI DHIDI YA WANAJESHI WA UINGEREZA (BATUK)

Madai ya mwanajeshi wa uigereza wanaofanya mazoezi humu nchini ya kumuua Agness Wanjiru 2012 yamepelekea familia yake kuilaumu idara ya upelelezi DCI na afisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma ODPP kwa kutatiza mchakato wa kupata haki. Akiwa mbele ya kamati ya bunge la kitaifa ya ulinzi msemaji wa familia hiyo Esther Muchiri amezishutumu idara […]

KAUNTI ZATAKIWA KUTHIBITI MAAMBUKIZI YA MPOX

Serikali za kaunti zimetakiwa kuimarisha ufuatiliaji ili kuthibiti kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa wa mpox. Waziri wa afya Debora Mulongo amesema kuwa serikali ya kitaifa iko macho kuhakikisha visa ibuka vinathibitiwa ili kumwondolea mkenya hofu na unyanyapaa unaohusishwa na ugonjwa huo. Imetayarishwa na Janice Marete

WAFANYIKAZI WA UMMA WAPATA NYONGEZA YA MISHAHARA

Ni afueni kwa wafanyikazi wa umma baada ya serikali kutoa kima cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya kuongezwa mishahara kwao. Serikali imechukua hatua hiyo kuzuia mgomo ambao wafanyikazi hao walikuwa wametishia kugoma mwishoni mwa mwezi hu una ambao ungeathiri pakubwa huduma mbali mbali za serikali. Waziri wa huduma za umma Justine Muturi anasema kuwa […]